Mkuu wa mkoa wa Singida
Dk. Parseko Vicent Kone amesema hayo katika hotuba yake iliyo somwa
na mkuu wa wilaya ya Singida, Bwana Said Amanzi katika hafla
ya kukabidhi mradi wa uboreshaji wa miundombinu rafiki kutoka shirika la Koica la
nchini korea,na kusema kuwa mashirika kutoka mataifa mengine
wame weza kuchangia na sisi watanzania inatubidi kuchangia
kwani jukumu la kuwalinda walemavu wangozi ni ni la watanzai wenyewe na
kuhakikisha wana pata ulinzi na elimu kama watu wengine.
Kwa
upande wake meneja mradi wa kujitolea kutoka shirika la Koica nchini
korea Bi. Park Jieun amesema mradi wa uboreshaji wa
miundombinu katika chuo cha ufundi na marekebisho kwa watu wenye
ulemavu sabasaba umegarimu zaidi ya shilingi milioni arobaini
na mbili kwa ajili ya kuboresha mazingira ya chuo kwa kujenga mabweni,matanki
ya maji na kuwasaidi walemavu ili waweze kuishi kama watu wengi
ambao siyo walemavu.
Awali mkuu
wa chuo cha ufundi na marekebisho kwa watu wenye ulemavu cha
sabasaba Bi. Fatuma Malenga ameiomba serekali kuangali uwezekano wa kukijengea
uzio chuo na kuweka vivuko maalumu pamoja na alama katika
barabara ambayo ipo karibu na chuo ili kuwawezesha wenye ulemavu wa ngozi na walemavu
wengine kuishi katika mazigira salama.
Akishukuru Bi.Jo Yunsil
Chilly kutoka shirika la Koica ambaye alikuwa akisimamia ujenzi wa mabweni na
miundo mbinu ya maji amesema kila mtu mwenye ulemavu ana haki sawa
kama wengine wasio kuwa walemavu kwa kupata elimu,kazi na kuwa na maisha kama
watu wengine,pamoja na jitihada walizo toa katika chuo hicho wana amini kuwa zita
wasaidia wananchi kuongeza utoaji wa elimu kwa walemavu.
0 comments:
Post a Comment