Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto limezindua mfuko
mpya wa kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia mamilioni ya watoto kwenye nchi
maskini zaidi duniani kuondokana na utapiamlo na hivyo kufikia ukuaji wa kiafya
unaoakiwa.
Uzinduzi huo umefanyika Washington, DC
kando mwa vikao vya Benki ya Dunia ambapo UNICEF imesema kupitia mfuko huo
uliopatiwa jina la Uthabiti wa lishe au The Power of Nutrition, nchi nufaika
zitaweza kuanzisha au kuimarisha programu zao za lishe ili hatimaye kujenga
jamii zenye afya na ustawi.
UNICEF inasema ushahidi unaonyesha kuwa
lishe bora utotoni ni msingi wa ukuaji bora kimwili na kiakili na hivyo ni
uwekezaji wenye manufaa makubwa.
Mfuko huo unaoweka dhahiri ushirikiano
kati ya sekta ya umma na binafsi unaungwa mkono na wadau mbali mbali wakiwemo
wahisani binafsi, mashirika ya kimataifa ya maendeleo na lengo ni kufikia dola
Bilioni Moja.
Dola Milioni 200 za awali zinatoka kwa
wadau kama vile Benki ya dunia, Idara ya maendeleo ya kimatifa ya Uingereza na
taasisi ya mfuko wa uwekezaji kwa watoto .
0 comments:
Post a Comment