MKURUGENZI
Mtendaji wa Kampuni ya Reli nchini(TRL),Mhandisi
Kapallo Kisamfu amesimamishwa kazi
kupisha uchunguzi wa malipo ya Sh. Bilioni
230 ya mabehewa ya Mizigo yenye kasoro
pamoja na kufanya malipo ya mabehewa yote kabla ya kukamilika.
Akitangaza
maamuzi hayo ya kusimimishwa kwa Mkurugenzi
huyo leo jijini Dar es Salaam baada ya ripoti
ya kamati iliyoundwa na Waziri wa Uchukuzi (ambaye sasa ni Waziri wa Afrika
Mashariki), Dk. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Uchukuzi,Samwel Sitta amesema
ameshtushwa na malipo hayo kwani
yamekiuka manunuzi ya umma kwani mkataba
wake ulikuwa TRL ilipe nusu ya asilimia
50 lakini matokeo yake mabehewa
yamelipwa yote.
Amesema
mabehewa 120 yaliyofika nchini yakiwa yana
kasoro aliyazuia baada ya kubaini hivyo n lakini TRL ilikuwa imeshalipa fedha
yote katika mazingira hayo yanaonyesha mkataba
una dalili ya hujuma.
Waliosimamishwa
wengine ni Mhandisi Mkuu wa Mitambo TRL,Ngosomwile
Ngosomiles,Mhasibu Mkuu,Mbaraka Mchopa
,Mkaguzi Mkuu wa Ndani Jasper Kisiraga
pamoja na Meneja Mkuu Ferdinand Soka.
Kamati ya
uchunguzi kwa watendaji hao kwa kuidhinishwa
kwa kulipwa kwa mabilioni ya Shilingi
itaongozwa na Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
za Serikali (CAG),Taasisi ya Kupambana na
Rushwa (Takukuru),Mamlaka ya udhibiti wa
Ununuzi katika sekta ya Umma (PPRA),pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Waziri wa
Uchukuzi,Samwel Sitta akizungumza na waandishi
wa habari kuhusiana kuwasimamisha baadhi
ya watendaji wakuu wa kampuni ya Reli hapa nchini uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo jijini Dar
es Salaam.
Home
News
News Alert: Mkurugenzi mtendaji TRL asimamishwa kazi kwa tuhuma za malipo kinyume cha mkataba
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment