Image
Image

Mkutano wa afrika mashariki wenye lengo la kuimarisha biashara kati ya nchi wananchama umeanza katika mpaka wa mtukula (uganda/tanzania).


Mkutano huu ambao unafanyika kwa siku mbili tarehe 16-17 April 2015, una lenga kusikiliza kero za wafanya biashara wanaotumia mpaka huu, kwani mpaka huu wa mtukula ni moja wapo ya mpaka ambao umekuwa gumzo kwa wafanya biashara kutoka Uganda kuja Tanzania au kutoka Tanzania kwenda nchini Uganda.

Moja wapo ya matatizo makubwa yaliyopo ni utitiri wa vizuizi vya barabarani kwani kwa mfano halisi, kutoka mtukula hadi Bukoba vipo vizuizi vya barabarani maarufu kama BERIA 7 ambapo mtukula penyewe zipo beria 3 moja ikisimamiwa na TRA, ya pili ikisimamiwa na Halmashauri ya wilaya ya Missenyi na ya tatu ikisimamiwa na Jeshi la Polisi. Kyaka zipo beria 3.

Hata hivyo, mkoa wa Kagera unaongoza kwa kuwa na vizuizi vya barabarani (beria ) jambo ambao linatia hofu hata kisaikolojia kwanini uwepo wa vizuzi hivi. Waweza kufikiri kuwa ni kwa sababu ya kulinda usalama wa wananchi au wasafiri na mali zao, na pengine baadhu hufikiri kuwa na vizuzi vingi barabarani kunachochea ukuaji wa biashara!

Mkutano umehudhuria na wajumbe kutoka umoja wa Afrika Mashariki, wa Uganda na Tanzania. Baada ya mkutano huu wa Mtukula, mkutano mwingine utafanyika katika mpaka wa Sirari/ Isebania , katika mpaka wa Uganda na Kenya

Katika mkutano huo, Wafanyabiashara  na  wajasriamali  wanaofanya  shughuli  za  kibiashara  katika  mpaka  wa  Mtukula  unaounganisha  nchi  ya  Tanzania  na  Uganda  wameomba  mamlaka  zinazohusika  kuondoa urasimu  na  vikwazo  visivyo  vya  kiforodha  ili  kuwaondolea  usumbufu  kwenye  shughuli  zao  za  kila  siku.

Wito  huo  umetolewa  na  wafanyabiashara na  wajasriamali  hao katika  semina iliyofanyika  katika  ukumbi  wa  jengo  la  Afrika  Masharika liliopo  Mtukula  wamesema  kuwa  kuna  vikwazo  visivyokuwa  vya  kiforodha  katika  protoko   ya  soko  la  Afrika  Mashariki  vinasababisha  kuwaingizia  hasara  wajasriamali  kwani  hata  biadhaa  zao  hurabika  na  kupoteza  thamani  wakati  wanatumia  gharama  kuzitafuta  na  kuzizalisha.

Mjasiriamali  Kasongo Kitwana  Mirambo  kutoka  mkoani  Tabora  amesema kuwa  amelazimika kuishia mpakani   na  lengo  lake  lilikuwa  auze  karanga  zake  tani  kumi nchini   Uganda  lakini  ameshindwa  baada  ya kuwepo  vikwazo  ambavyo  katika  maelezo    na  protoko  ya  soko  la  Afrika  Mashariki  havijaainishwa  kwenye  sheria  hivyo  vimemsababishia  hasara  kubwa  na  kumwalibia  malengo  yake.

Pia  amelalamikia ushuru  unaotozwa  kwenye  bidhaa  zinazosafirishwa  akitolea  mfano  kuwa  wakati anatokea  mkoani  Tabora  alilipia  ushuru wa  mazao lakini  alitozwa  tena  ushuru  wa  mazao  alipofika  Mtukula na  kuongeza  kuwa  huko  ni kumukandamiza  mjasriamali  na  hawezi  kupata  faida  na  kufaidi  uwepo  wa  soko  la  pamoja  la  jumuia  ya Afrika  mashariki.

Ibrahimu  Sekwaro  ambaye  ni  mmiliki  wa  shule  ya  Lake View  iliyopo  Bukoba  amesema  kuwa kwa  Tanzania  kuna  mlolongo  mrefu  unaoleta  usumbufu  kwa  wataalamu  kama  walimu wanaotaka  kuja  nchini kufundisha  kutoka  nchi jirani  ambazo  ni  mwanachama  wa  Jumuia  mashariki  wakati  protoko  ya  soko  la  pamoja  limeelekeza  watu  wenye  ujuzi  na  kazi  ataweza  kuajiriwa  bila  vikwazo.

Amesema  wakati  nchi  nyingine mwanachama  wakitoa  fursa  hiyo  kwa  unafuu  hali  ni  tofauti  Tanzania  ambapo   mtu  anayetaka  ajira  hiyo  hulazimika  kutafuta  kibali  cha  ajira  na  vinapatikana  kwa gharama  ya  juu zaidi  na  kupitia  wizara  tatu  tofauti  mfano  wizara  ya  mambo  ya  ndani,wizara  ya  Elimu  na  mafunzo  ya  ufundi  na  wizara  ya  kazi  hali  inayochangia kukosa  wataalamu   wakati  nchi  nyingine  zikifaidika  na  soko  la  pamoja la  jumuia  ya  Afrika mashariki.

Sekwaro pia  ametolea  mfano wa  ushuru  wa  kodi  ya  forodha unaotozwa kwenye  karatasi  zinazoagizwa  kutoka  nchi  mwanachama  katika  Jumuia  ya  Afrika  Mashariki  Kenya  kuwa  zipo  juu  sana  na  wakati  nchi  ya  Uganda  inatoza  ushuru  nafuu  na  kuwezesha  upatikanaji  rahisi  wa  bidhaa  hiyo.

Kwa  upande  wake  Rwechungura  Mali  ambaye ni Afisa  Mtendaji  wa chama  cha  wafanyabiashara  mkoa  wa  Kagera  TCCIA  amesema  kuwa  kuna  vikwazo  vingi  katika  mpaka  wa  Mtukula  na  kuna  baadhi  ya  watendaji  wa  Chakula  na  Dawa TFDA ,Kilimo  na  wengineo  wanafanya  ubadilifu  walipisha  wafanyabiashara   ushuru  lakini  hawatoi  stakabadhi  za  malipo.

Wakichangia  mjadala  Afisa  wa  Mamlaka  ya  Mapato  amesema  kuwa  wanatoza  ushuru  kwa  kufuata  mwongozo  wa  jumuia  ya  Afrika  Mashariki  jibu  ambalo  halikuweza  kukidhi kiu  ya  wafanyabiashara  na  wajasrimali  waliohudhuria  semina  hiyo.

Hata  hivyo wajasriamali wametakiwa  kufuata  taratibu  na  kanuni  za  kuwa  na  vibali  husika  ili  kuepusha  kutapeliwa  na  kupata  hasara  kwa  kukosa  utambulisho  halali  wanapokuwa nchi  nyingine  za  jumuia.

Semina  ya  hii  imewezeshwa  na  mwezeshaji  toka  nchini  Rwanda  Christine   Mukangoboka, wengine  ni Robi  Ernest  Bwiru   kutoka  katika  wizara  ya  Afrika ya  Mashariki  nchini  Tanzania  na  wengine  ni  maafisa  kutoka  makao  makuu  ya  jumuia  ya  Afrika  Mashariki  Arusha  na wengine  kutoka wizarani  nchini  Uganda.

JUHUDI fELIX 0756 601054                                                                                                         Chanzo:Fadeco
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment