Image
Image

Mkuu wa mkoa wa kigoma awaongoza mamia ya waombolezaji kuaga ndugu na jamaa zao waliofariki kwa kupigwa na radi Kigoma Ujiji.


Mkuu wa mkoa wa kigoma Luten Kanal Mstaafu Issa Machibya  amewaongoza mamia ya wakazi wa manispaa ya kigoma ujiji  kuaga miili ya watu wanane wakiwemo wanafunzi  sita wa darasa la kwanza katika shule ya msingi ya kibirizi mjini kigoma walio fariki dunia jana baada ya kupigwa na radi kufuatia mvua iliyonyesha kwa takriban masaa matatu.
Akitoa salam za rambirambi mkuu wa mkoa wa kigoma Luten Kanal Mstaafu Issa Machibya amewataka wafiwa na wananchi kuchukulia  tatizo hilo kama ni tukio la ajali ya kawaida na kwamba msiba huo ni mzito.
Majonzi yalitawala shughuli hiyo  hasa baada ya miili hiyo kupokelewa katika viwanja  vya  shule ya msingi kibirizi kabla ya ndugu kukabidhiwa tayari kwa maziko huku mwili wa Mwalim Elieza Mbwambo ukisafirishwa kwenda moshi kwa maziko .

Kwa upande wao viongozi wa dini Shekh Moshi Guoguo kutoka Bakwata na mchungaji Emmanuel Mtoi wa kanisa la KKKT wakitoa mawaidha katika msiba huo, wamewataka waumini wa dini mbalimbali kujiandaa kwa kuwa kila mwanadamu ataonja mauti  kwa wakati wake na kwamba imani za kishirikina zisihusishwe katika msiba huo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment