Image
Image

Mtandao wa vibaka na uhalifu wajiimarisha maeneo mengi nchini




Pamoja na kuendelea kuvutia misururu ya watu wanaoingia katika Jiji la Dar es Salaam kila kukicha, maeneo yake mengi yamebainika kuwa si salama.

Uchunguzi uliofanywa na timu ya waandishi wa Mwananchi katika maeneo mbalimbali yanayotajwa kwa uporaji, umethibitisha kuwapo kwa matukio ya wizi na uporaji kwa kutumia mbinu mpya zinazobuniwa na vibaka kila kukicha.
Maeneo hatarishi ambayo yamebainika katika uchunguzi huo ni pamoja na Buguruni, Kinondoni, Tandale, Msasani, Mwananyamala, Ubungo, Temeke na hata maeneo ya ‘uzunguni’.
Katika maeneo yaliyofanyiwa uchunguzi, zimebainika aina na mbinu tofauti za wizi, ukiwamo wa simu na maeneo zinapouzwa.
Mbinu hizo ni vibaka kujifanya wanafanya mazoezi ya kukimbia na kuwakwapua mikoba na kompyuta wapitanjia. Pia wapo wanaofanya hivyo kwa kutumia pikipiki na magari. Wapo pia wanaojifanya wanaongoza magari na wengine kujifanya wanajitolea kukarabati barabara.
Eneo la Mkwajuni limekuwa na matukio mbalimbali ya kihalifu ikiwamo ukabaji na uporaji wa vitu na mali za watembea kwa miguu.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kawawa, Elizabeth Massawe anasema: “Mwaka jana hali ilikuwa mbaya zaidi na watu walikuwa wanakabwa sana. Lakini kuanzia Januari mpaka Machi kuna watu watatu tu ndiyo waliokutwa wamekufa katika Bonde la Mkwajuni, kuna vijana wawili wa kiume na mwanamke mmoja aliyeuawa na kutupwa chini ya Daraja la Mto Ng’ombe hapo bondeni.”
Massawe anataja sababu ya kukithiri kwa matukio hayo kuwa ni pamoja na eneo hilo lenye vichaka na uwazi mkubwa, kuwa mbali na makazi ya watu… “Kwa hivyo inakuwa rahisi vibaka kufanya uhalifu, lakini tayari nimeshaunda kikosi cha ulinzi shirikishi ambacho kinaendelea na kazi ya kuimarisha ulinzi.”
Mjumbe wa Mtaa wa Mkunguni B, Rajabu Omary anasema mpaka sasa hakuna usalama wa watu kutembea kwa miguu katika eneo la bonde hilo kutoka Magomeni au Kinondoni Studio.
“Kuanzia saa 12.00 jioni hutakiwi kutembea kwa miguu kama unahitaji kuwa salama, vinginevyo utakuwa unatengeneza ushawishi wa kufanyiwa uhalifu. Ulinzi wa polisi hauwezi kufika mpaka huku, lakini sisi na jamii kwa pamoja tunatakiwa kuwa walinzi kwa kila mmoja wetu.”
Maeneo hayo ambayo siyo salama, yanajumuisha eneo la Kinondoni Studio na kwa Manyanya.
Licha ya kukithiri kwa wizi, maeneo hayo yanatumika pia kama kichaka cha wahalifu hao. Vibaka wengi baada ya kuiba hukimbilia barabara za Morogoro na Kawawa kwenye mabonde ya Jangwani na Mkwajuni kujificha.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment