Mtu mmoja amefariki dunia baada ya kugongwa vibaya na treni wakati akivuka reli na kisha viungo vyake kusambaa katika mtaa wa ujenzi manispaa ya morogor.
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema marehemu alijulikana kwa jina moja la
mangi ambapo wameeleza kusikitishwa na ajali
kwakua hii ni mara ya tatu watu kugongwa na treni katika
maeneo hayo na kueleza kuwa amarehemu alikua anavuka Reli.
Naye mwenyekiti wa mtaa
wa ujenzi Christopha Chales ameelezea tukio hilo na
kuwataka wananchi kuacha tabia ya kupita kwenye njia ya Reli kwani
wataendelea kusababisha ajali zisizo za lazima ambazo
zingeweza kuepukika.
Askari wajeshi la polisi
wamefika katika eneo la tukio na kuchukua mwili wa
marehemu ambapo umehifadhiwa katika chumba cha maiti katika
hospitali ya rufaa ya mkoa wa morogoro .
0 comments:
Post a Comment