Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba
amebainisha sababu nne zinazowafanya wananchi wampendekeze kugombea urais
katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Nchemba aliyasema hayo kwenye mahojiano
wakati wa kipindi cha dakika 45 kinachorushwa na ITV kuhusu tafiti zinazofanywa
juu ya kukubalika kwa baadhi ya watia nia ya urais miongoni mwa wananchi
wanaomtaja.
“Nisingependa kuwa refarii na mchezaji kwa
wakati mmoja katika hili. Kuna ripoti iliwahi kuonyesha kuwa ninaongoza katika
mbio hizo kwa kupata asilimia 37 na nyingine ikasema nimeshika nafasi ya pili.
Ninawashukuru wananchi wanaoona kuwa nafaa katika nafasi hiyo.”
Aliongeza: “Wanaonipigia kura wanaona nidhamu
katika usimamizi wa ukusanyaji wa mapato, matumizi. Pia mabadiliko ya kukomesha
ufanyaji kazi wa mazoea.”
Tangu ateuliwe kushika wadhifa wa Unaibu
Waziri, Nchemba alisema amefanya mabadiliko kadhaa ambayo yamesaidia kudhibiti
matumizi ya Serikali, ikiwamo kupitisha malipo ya wafanyakazi wote wa serikali
katika akaunti zao za benki.
Sambamba na hilo aliagiza wakuu wa idara wote
kuhakiki taarifa za watumishi walionao katika ofisi zao jambo lililochangia
kuokoa zaidi ya Sh400 milioni zilizokuwa zinalipwa kwa waajiriwa hewa.
Pamoja na hayo alisema kuwa, kwa sasa
amejikita zaidi katika kutekeleza majukumu yake ya unaibu waziri.
Alipoulizwa anachukuliaje kufananishwa na
aliyewahi kuwa waziri mkuu katika utawala wa awamu ya kwanza, Edward Sokoine,
alijibu kuwa hiyo ni ishara nzuri kwani kiongozi huyo alitukuka katika utumishi
wa umma.
“Hilo linanifanya nitende kulingana na
mahitaji ya wananchi. Uongozi wa Sokoine ulipendwa na wengi na kufananishwa na
kiongozi aliyetukuka kama yeye ni sifa nzuri inayoniongezea ari,” alisema.
Kuhusu kuvaa viatu vyake, Sokoine alibainisha
kuwa hilo bado kwani nafasi anayohudumu hailingani na ile aliyokuwa nayo
Sokoine.
Akizungumzia mtindo wake wa kuvaa skafu ya
bendera ya Taifa alisema, anatazamia kuwa baada ya muda mfupi itakuwa ni
utambulisho wa taifa kwa kila Mtanzania atakayeenda nje ya nchi.
“Nilianza kuvaa skafu tangu nikiwa sekondari…wakati
huo zenye rangi za bendera ya taifa hazikuwa nyingi lakini kadri siku
zinavyosogea zinaongezeka.
Viongozi wakubwa Afrika walikuwa na mavazi
yaliyowatambulisha,” alisema akitolea mfano marais Keneth Kaunda wa Zambia na
Kwame Nkurumah wa Ghana.
Akifafanua kuhusu mpango wa Serikali kuongeza
mapato na migomo ya wafanyabiashara ya mara kwa mara inayoendelea alisema kuwa
inachafua sifa nzuri ya Taifa.
Home
News
News Alert: Nchemba abainisha sababu kuu nne za msingi zinzofanya wananchi kumpendekeza kugombea urais mwaka huu.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment