Image
Image

News Alert: Kijana mmoja aliyepatikana na hatia ya kulawiti mwanafunzi wa kike wa miaka 9 ahukumiwa miaka 30 jela Tabora.


Mahakama  ya wilaya ya Tabora imehukumu  Masudi Nassor  mkazi wa kata ya kiloleni manispaa ya Tabora (20) kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya ulawiti kwa mwanafunzi wa kike wa shule ya msingi mwenye umri wa miaka 9.
Akitoa hukumu hiyo hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Tabora mjini, Mhe. Bahati Chitepo amesema kwamba ametoa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye nia kama hiyo kwa watoto, na jamii ijifunze kutoka kwake.
Awali mwendesha mashitaka wakili wa serikali bw. Miradi kijulu amesema kuwa, mshitakiwa (MASOUD NASORO) alitenda kosa hilo eneo la kata ya kiloleni ambapo muathirika wa tukio hilo alimuomba lifti akiwa anakwenda shuleni na ndipo mshitakiwa alimpeleka vichakani mtoto huyo eneo la kalunde  na kumfanyia unyama huo.
Baada ya kutenda kosa hilo mshitakiwa alikimbia hadi alipotiwa nguvuni na jeshi la polisi na kufikishwa mahakamani,hata hivyo mshitakiwa huyo aliiomba mahakama hiyo impunguzie adhabu kwani anaishi na babu yake mlemavu wa mguu na wazazi wake wote wamafariki dunia, maombi ambayo yaliyupiliwa mbali.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment