Image
Image

News Alert:Kamati ya bunge ya Ardhi na mali Asili ya Tanzania yaipongeza Afrika kusini kwa kutumia rasilimali zake vizuri.


Na.Ignas Mwaipesa.Afrika Kusini.
Kamati ya Bunge ya ardhi,maliasili na mazingira ya Tanzania imeipongeza afrika kusini kwa kutumia rasilimali zake vizuri kujenga mundombinu bora ya kuwezesha watalii kufika katika ncha ya kusini kabisa ya bara la afrika iitwayo CAPE POINT licha ya barabara hizo kupita katika maeneo hatari ikiwemo milima  na majabali makubwa ya mawe katika mwambao wa bahari ya ATLANTIC.
Wakiongea baada ya kufika katika ncha hiyo ya kusini ya bara la afrika ambapo pia bahari mbili hukutana yaani bahari ya hindi yenye maji ya joto na bahari ya ATLANTIC yenye maji baridi,wajumbe wa kamati hiyo akiwemo mwenyekiti wake JAMES LEMBELI na DK PETER KAFUMU wamesema licha ya kwamba barabara hizo zinapita kwenye milima hiyo ya hatari lakini nchi hiyo kwa kutumia rasilimali zake imezijenga kwa ustadi mkubwa na kuwezesha safari za watalii kuwa za usalama.
Nao baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo ya bunge walioko kwenye ziara hiyo ya mafunzo nchini afrika kusini wamesema uwekezaji mkubwa katika sekta hiyo, umeiwezesha nchi ya afrika kusini kuwa ya pili kwa idadi kubwa ya watalii barani afrika baada ya misri watalii ambao wanaliwezesha taifa hilo kupiga hatua kubwa kwa maendeleo ikilinganishwa na tanzania ambayo imekuwa ikipata watalii wachache kwani licha ya kuwa na maliasili nyingi lakini miundombinu yake haijawa rafiki kwa watalii.
Kamati hiyo ya bunge pia imefika katika eneo la CAPE OF GOO HOPE ama Rasi ya tumaini jema maeneo ambayo wavumbuzi wa kale akiwemo VASCO DAGAMA na BATHOLMEW DIAZ walifika mwanzoni mwa miaka ya 1800 wakiwa katika harakati za kufika india kwa njia ya bahari kutokea afrika ambao pia walijenga minara kuyatambulisha kama maeneo muhimu kimataifa na nchi ya afrika kusini imeyafanya kuwa sehemu ya hifadhi ya taifa ya milima meza au TABLE MOUNTAIN ambayo ni miongoni mwamaajabu saba ya asili ya dunia.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment