Image
Image

News Alert: SERIKALI imesema hakuna mtanzania aliefariki kwa vurugu za afrika kusini.

SERIKALI imesema hakuna mtanzania aliyepoteza maisha kwa vurugu zinazoendelea nchini Afrika Kusini kutokana na wenyeji wa nchi hiyo kuwachukia wageni.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe amesema watanzania waliofariki nchini Afrika Kusini hawatokani na vurugu za wenyeji kuwakataa wageni.
Membe amesema tatizo hilo lilianza 2008 na 2014 hiyo lilichangiwa na Mfalme wa nchini humo kuchochea fujo hizo dhidi wageni lakini Mfalme huyo amejitokeza leo na kuzungumza na wananchi hao kwa kuwaasa kuacha kuwaua wageni waliopo nchini humo.
Amesema watanzania waliopo katika makambi ni watanzania 23 ambao wawili wamekataa kurudi na 21 wanasema wanaweza kurudi hivyo mpango wa kuwarudisha nyumbani unafanyika na serikali ina uwezo huo.
Amesema watanzania walioko katika mataifa mbalimbali wajenge tabia ya kujiandikisha katika balozi zao pamoja na kuunda umoja ili kuweza kupata taarifa panapotokea matatizo.
Hata hivyo amesema serikali imekuwa ikifanya mazungumzo ya karibu na viongozi wa nchini Afrika Kusini juu vurugu hizo na taarifa zimekuwa nzuri.
Membe amesema kunahitajika kujenga uchumi imara katika nchi za Afrika ili kuwezesha vijana wengi kuajiriwa na kujiajiri na kuachana na kukimbilia katika nchi hizi zenye uchumi wakati hawana ujuzi.
Membe amesema Mwenyekiti wa Jumuiya ya Nchi zilizopo Kusini mwa Jangwa la Sahara (SADC),Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU),Robert Gabriel Mugabe amelaani kitendo hicho.
Aliwataja watanzania waliopoteza maisha nchini Afrika Kusini kwa sababu tofauti na vurugu hizo, kuwa ni Rashid Jumanne aliyeuawa kutokana na kufanya unyang'anyi,Athuman China aliechomwa kisu akiwa gerezani kwa vurugu,Ally Mohamed alikuwa na ugonjwa wa kifua kikuu TB na mwili wake umeletwa nchini jana kutoka Afrika Kusini.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment