SERIKALI imesema hakuna mtanzania aliyepoteza maisha kwa vurugu
zinazoendelea nchini Afrika Kusini kutokana na wenyeji wa nchi hiyo kuwachukia
wageni.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe amesema watanzania waliofariki nchini
Afrika Kusini hawatokani na vurugu za wenyeji kuwakataa wageni.
Membe
amesema tatizo hilo lilianza 2008 na 2014 hiyo lilichangiwa na Mfalme wa nchini
humo kuchochea fujo hizo dhidi wageni lakini Mfalme huyo amejitokeza leo na
kuzungumza na wananchi hao kwa kuwaasa kuacha kuwaua wageni waliopo nchini
humo.
Amesema
watanzania waliopo katika makambi ni watanzania 23 ambao wawili wamekataa
kurudi na 21 wanasema wanaweza kurudi hivyo mpango wa kuwarudisha nyumbani
unafanyika na serikali ina uwezo huo.
Amesema
watanzania walioko katika mataifa mbalimbali wajenge tabia ya kujiandikisha
katika balozi zao pamoja na kuunda umoja ili kuweza kupata taarifa panapotokea
matatizo.
Hata hivyo
amesema serikali imekuwa ikifanya mazungumzo ya karibu na viongozi wa nchini
Afrika Kusini juu vurugu hizo na taarifa zimekuwa nzuri.
Membe
amesema kunahitajika kujenga uchumi imara katika nchi za Afrika ili kuwezesha
vijana wengi kuajiriwa na kujiajiri na kuachana na kukimbilia katika nchi hizi
zenye uchumi wakati hawana ujuzi.
Membe
amesema Mwenyekiti wa Jumuiya ya Nchi zilizopo Kusini mwa Jangwa la Sahara
(SADC),Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU),Robert Gabriel Mugabe amelaani
kitendo hicho.
Aliwataja
watanzania waliopoteza maisha nchini Afrika Kusini kwa sababu tofauti na vurugu
hizo, kuwa ni Rashid Jumanne aliyeuawa kutokana na kufanya unyang'anyi,Athuman
China aliechomwa kisu akiwa gerezani kwa vurugu,Ally Mohamed alikuwa na ugonjwa
wa kifua kikuu TB na mwili wake umeletwa nchini jana kutoka Afrika Kusini.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment