Image
Image

Serikali imewataka viongozi waserikal ya Lamadi kuwatafutia wahanga wa mafurika maeneo mengine ya kuishi.


Serikali mkoani Simiyu imewaagiza viongozi wa serikali ya kijiji cha Lamadi kilichoko wilayani Busega mkoani simiyu ambao walikumbwa na mafuriko wiki iliyopita na kusababisha nyumba zao kusombwa na maji  kuwatafutia maeneo mengine ya kuishi wananchi hao.
Agizo hilo limetolewa na mkuu wa mkoa huo,Elaston Mbwilo Katika kijijiji cha lamadi wakati alipokwenda kuwatembelea wananchi hao waliokumbwa na mafuriko hayo ambapo amesema eneo hilo kwa hivi sasa halifai tena kwa makazi kwani wananchi wakiachwa wakaendelea kuishi hapo kila mwaka watakuwa wanakumbwa na mafuriko kutokana na mabadiriko ya tabia nchi.
Aidha mkuu huyo wa mkoa amewaomba wananchi hao kuendelea kuwa na subira kwani serikali bado inaendelea kufanya tathimini ya mafuriko hayo  na kwamba ikikamilisha watalewa chakula ambapo pia amewaomba wasamalia wema,mashairika na taasisi zilizoguswa na janga hilo kuendelea kutoa misaada kwa wananchi hao.
Wiki iliyopita wananchi wa kijiji hicho walikumbwa na mafuriko ambapo nyumba 288 zilibomolewa,baadhi ya mifugo kama kondoo na kuku kusombwa na maji huku zaidi ya kaya 1686 zikiwa hazina mahali pa kuishi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment