Image
Image

SerikalI kuwachukulia hatua viongozi wa kisiasa watakao tumia majukwaa ya siasa washawishi wananchi kutochangia ujenzi wa maabara


SERIKALI wilayani Bunda imesema italazimika kuchukua hatua kali zikiwemo za kisheria  kwa viongozi wakiwemo  wa kisiasa ambao watabainika kuitisha mikutano hasa katika  maeneo ya vijijini na kuwashawishi wananchi kutochangia ujenzi wa maabara katika shule za sekondari wilayani humo.
Ujenzi huo wa maabara ni utekelezaji wa agizo la  Rais Jakaya Mrisho Kikwete,ambaye  ametaka kila kila mkuu wa wilaya kusimamia ujenzi wa maabara tatu katika shule zote za  sekondari.

Agizo hilo la serikali wilayani bunda limetolewa na mkuu wa wilaya hiyo Bw.Joshua  Mirumbe,baada ya kupokea mifuko mianne ya saruji ambayo imetolewa na mmoja ya wakazi wa  bunda kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba 81 vya  maabara katika shule  27   za sekondari wilayani Bunda.

Kwa upande wake Mkazi huyo wa bunda ambaye pia ni mkurugenzi wa kampuni ya Mwanza Huduma  ya jijini mwanza Bw Zully Nanji,akizungumza baada ya kukabidhi sheena hiyo ya mifuko ya  saruji,amesema kuwa kama mzawa wa wilaya  ya bunda,ameguswa katika  kuchangia ujenzi wa miundombinu ya elimu kwa ajili ya  kuharakisha maendelea ya  jamii na taifa kwa ujumla.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment