Wakazi wa wilaya ya
muheza wameishauri tume ya taifa ya uchaguzi kuahirisha zoezi la
kuipigia kura rasimu ya pili ya katiba na badala yake isubiri hadi
uchaguzi mkuu wa rais na wabunge ufanyike kufuatia idadi kubwa ya watanzania
kudai kuwa muda uliowekwa ni mdogo wa kuipitia na
kuipitisha rasimu ya pili pendekezwa.
Wakizungumza katika
mkutano wa hadhara ulioitishwa kituo cha sheria na haki za binadamu kwa
kushirikiana na tume ya taifa ya uchaguzi wakazi hao wamesema mapendekezo mengi
waliyowasilisha katika rasimu ya kwanza ya katiba kwa mwenyekiti wa tume hiyo
jaji joseph sinde warioba yamepunguzwa hivyo ni lazima tume ijipange upya
ili kuleta demokrasia ya kweli nchini.
Kwa upande wake mwenyekiti
wa wazee wa wilaya ya Muheza akielezea suala ya uhesabiaji wa kura
mara baada ya ya siku yaupigaji kura katka katiba pendekezwa
kufika,ameiomba tume ya taifa kufanya mabadiliko kwa waratibu wa uchaguzi ambao
ni wakurugenzi wa halmashauri katika mchakato huo na badala yake
watafutwe watu wa makundi tofauti yenye heshma kwa sababu watakosa
imani ya kupata takwimu sahihi za waliopiga kura ya hapana na ndio .
Kufuatia hatua hiyo
mratibu wa kampeni ya utoaji elimu kwa wananchi kuhusu rasimu ya
katiba wa kituo cha sheria na haki za binadamu mkoa wa
tanga Bwana. Stanley Gumbo amewataka wananchi kuzingatia elimu ya katiba
zoezi hilo la kitaifa lengo lake ni kutaka wananchi wakubali kwa ridhaa yao ili
kupata katiba mpya.
0 comments:
Post a Comment