Akiongea katika hospital ya Kagondo mganga mkuu wa hospitali
ya rufaa ya mkoa wa Kagera Thomas Ruta amewataka akinamama wajawazito kufika
katika vituo vya afya mara kwa mara ili waweze kuchunguzwa afya zao na
kuongeza kuwa hospital ya kagondo imekuwa na umuhimu mkubwa katika mkoa
huo na taifa kwa ujumla kwani kutokana huduma bora zinazo tolewa katika
hospital hiyo kumesaidia kuipunguzia mzigo hospitali ya rufaa ya mkoa wa
kagera ambayo ilikuwa ikipokea mamia ya wagonjwa kutoka sehemu mbalimbali kila
kukicha.
Kwa upande wake Rais na mkurugenzi mtendaji wa shirika
lisilokuwa la kiserikali la Jhpigo kutoka nchini marekani ambalo
limekuwa likijishughuli katika kutoa huduma za afya ya uzazi kwa akina mama na
watoto walio chini ya miaka mitano Leslie Mancuso ameridhishwa kwa kiasi
kikubwa na huduma zinazotolewa kwa akinamama na watoto katika hospital ya
hospital hiyo na kwamba shirika hilo sasa lita jikita zaidi katikakuongeza
vifaa tiba katika hospital hiyo ikiwemo huduma ya usafiri kwa wagonjwa
kwaajili ya kunusuru vifo kwa akinamama wajawazito na watoto.
Nae muunguzi afisa muunguzi wa wodi ya akinamama
wajawazito PASCHAZIA HENRY amesema pamoja na huduma zinazotolewa
katika hospitali lakini bado kuna changamoto nyingi ikiwemo
upungufu wa wahudumu kwani kunawakati wanapokea wagonjwa wengi
kupita kiasi huku katibu wa hospital hiyo JOSHUA JOSEPH akiwataka
akina mama wajawazito kuepukana na imani potofu za kutumia dawa za
kuongeza nguvu ya uchungu wakati wakujifungua kwani zimekuwa zipelekea vifo kwa
akinamama wengi nchini badala yake wafike katika hospital pamoja na vituo mbali
vya afya ili waze kupata ushauri nasaa juu ya afya ya uzazi
kwa mama na watoto.
0 comments:
Post a Comment