Image
Image

Wanafunzi 290 Nangombo-Nyasa washindwa kusoma kwa wiki tatu kwa kukosa chaki za kufundishia


Na. Emmanuel Msigwa,Songea.

Zaidi ya wanafunzi 290 wa shule ya msingi ya Nangombo katika wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma,wameshindwa kuhudhuria masomo yao Darasani kwa wiki tatu kutokana na kukosa chaki za kufundishia hali ambayo inatishia pia wanafunzi wa Darasa la saba wanaokabiliwa na mtihani wa mwisho mwaka huu kutofanya vizuri.

 Kwa zaidi ya wiki tatu mfululizo wanafunzi wakiwemo wa Darasa la Saba katika shule hii ya msingi ya Nangombo iliyopo makao makuu ya wilaya ya Nyasa, wameshindwa kusoma kutokana na walimu kukosa chaki za kufundishia hali ambayo imemstajaabisha pia kamanda wa vijana-CCM katika wilaya hiyo,Bwana CASSIAN NJOWOKA aliyetembelea shule hiyo. 

Kutokana na tatizo hilo, Bwana NJOWOKA mbali ya kukabidhi BOX 25 za chaki kwa shule hiyo, pamoja na kuahidi kuwalipa posho walimu watakaofundisha wanafunzi wa darasa la saba hadi siku ya mitihani yao, pia anasema atajitolea kuwapeleka Dar es salaam vijana sita kujifunza namna ya kutengeneza chaki ikiwa ni pamoja na kununua mashine mpya ya kuzalisha chaki hizo ili ziweze kuondoa tatizo la chaki kwa shule zote za wilaya ya Nyasa.

Kwa mujibu wa maelezo ya mwalimu mkuu wa shule hii ya msingi Nangombo,Bwana Yasint Hyera, shule hii ipo katika himaya ya wamision wakatoriki hivyo wametafuta eneo lingine la kujenga shule mpya huku kamanda huyo wa vijana CCM wilaya ya Nyasa akiwataka wananchi kujitolea kufyatua tofari na yeye atachangia BOX za marumaru pamoja na vifaa vyote vya kiwandani kwa madarasa mawili.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment