WATU wanane wakiwemo
wanafunzi sita wa shule ya msingi kibirizi Manispaa ya Kigoma wamekufa baada ya
kupigwa na radi kufuatia mvua kubwa iliyonyesha.
Mganga Mfawidhi wa
Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa kigoma Maweni,DK.FADHILI KIBAYA amesema sambamba
na watu hao waliofariki pia watu 15 wamejeruhiwa katika tukio hilo.
Dk.Kibaya amewataja
waliofariki kuwa ni pamoja na Yusuf Athuman, Hassan Ally, Fatuma Sley, Zamda
Seif, Shukrani Yohana na Warupe Kapupa ambao ni wanafunzi wa darasa la kwanza
katika shule hiyo ambapo Mwalim aliyefariki ametambuliwa kwa jina la Elieza
Mbwambo aliyekuwa akifundisha darasa la tano.
Aidha pamoja na watu hao
mtu mwingine aliyetambuliwa kwa jina la Focas Ntahamba pia amefariki kwa
kupigwa na radi katika eneo la Bangwe mjini kigoma.
Mmoja wa walimu wa shule
ya msingi ya kibirizi,WILBERT EMANUEL ambaye alikuwepo eneo la tukio amesema
kuwa wamesikitishwa na tukio hilo ambalo lilitokea bila kutegemea na kuacha
simanzi kubwa shuleni hapo.
Hili ni tukio la pili
kutokea mkoani kigoma ambapo takriban mwezi mmoja uliopita
wanafunzi sita na mwalim wao walikufa baada
ya kupigwa na radi katika shule ya msingi nyakasanda katika kijiji cha
nyachenda wilayani kasulu .
0 comments:
Post a Comment