Image
Image

Wizi wa vifaa vya magari na magari vya Ogofya Dar es Salaam

Wezi wa vifaa vya magari jijini hapa wameunda mtandao mzito kama vile wana ‘serikali yao’ inayowalazimisha waathirika kuacha kutoa taarifa polisi badala yake kwenda kununua upya vifaa kwa wezi hao.
Licha ya wizi wa vifaa, kumekuwa na wizi mkubwa wa magari Dar es Salaam kiasi kwamba mwaka 2013, magari yaliyoibwa ni 400. Mwaka 2014 yaliibwa 375 na kwa kipindi cha Januari hadi Machi mwaka huu magari 70 yameibwa.
Kutokana na hali hiyo, polisi jijini Dar es Salaam wamelaumiwa kwa kushindwa kutokomeza mtandao huo, licha ya wahusika kufahamika kwa majina, makazi na mahali wanakohifadhi vifaa hivyo vya wizi.
Hata hivyo, polisi nao kwa upande mwingine wametupa lawama kwa wananchi wanaoibiwa vifaa hivyo, kuwa hawatoi ushirikiano kwa jeshi hilo badala yake wameona njia rahisi ni kwenda kununua upya mali zao kwa wezi hao.
Uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa baadhi ya wananchi walioibiwa vifaa hivyo wanakataa kutoa taarifa polisi kwa kuhofia kupoteza muda, gari kubaki polisi kama kielelezo hadi vifaa vipatikane, kutakiwa kutoa fedha kwa wapelelezi au kuhisi kuwa baadhi ya askari wanahusika na mtandao huo.
Baadhi ya wakazi wa jiji waliowahi kuibiwa vifaa hivyo wamesema haichukui muda mrefu kwa mtu kubaini mahali vilipo na kuvipata tena, lakini kwa polisi wenye kila ujuzi kiupelelezi limeendelea kuwa tatizo.
Vifaa vinavyoibwa zaidi
Kutokana na uchunguzi wa gazeti hili, vifaa vinavyohitajika zaidi kwa sasa ni side mirror, control box, power window, vioo vya mbele na nyuma, taa, dash board, redio na baadhi ya vifaa vya injini.
Magari ambayo vifaa vyake vinaibwa zaidi ni yale yanayopatikana kwa wingi hasa aina ya Toyota na Suzuki, yakiwamo Escudo, Altezza, Mark II Grand, Cresta, Verossa, Noah, Ipsum, Klugger, Harrier, Vitz na Ist ambayo kutokana na wingi wake vifaa hivyo hupata wateja haraka.
Katika uchunguzi huo Mwananchi limebaini kuwa, watu wanaoharibikiwa magari, kugongwa au kuibiwa vifaa kwa siku ni wengi kwa hivyo wezi hupata uhakika wa kuuza vifaa hivyo.
Kauli ya polisi
Mkuu wa Upelelezi, Kanda ya Dar es Salaam, Constantine Massawe alipoulizwa sababu za kukithiri kwa tatizo hilo, alisema wizi wa vifaa vya magari unashughulikiwa kama uhalifu mwingine, lakini jeshi hilo halipati ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wananchi wanaoibiwa vifaa hivyo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment