Toure
amebakiza miaka miwili katika mkataba wake wa sasa ambao unampatia kitita cha
Pauni 220,000 kwa wiki na staa huyo hataki kwenda katika klabu nyingine ambayo
itampatia mshahara chini ya huo. Klabu nyingi kubwa Ulaya ikiwemo Inter Milan
zinavutiwa na mpango wa kumchukua staa huyo lakini zinachoshwa na mshahara wake
mkubwa ambao unamfanya kuwa mmoja kati ya wachezaji wanaolipwa sana Ulaya.
Inter
Milan inadaiwa ipo tayari kumpa mkataba wa miaka mitano kufidia punguzo la
mshahara wake wa sasa lakini haionekani kama Toure atakubali wazo hilo.
Mkurugenzi
wa Ufundi wa Inter Milan, Piero Ausilio hivi karibuni alikiri kwamba klabu yake
bado ina ndoto za kumnyakuwa Toure ambaye aliwahi kufundishwa na kocha wao wa
sasa, Roberto Mancini wakati akiwa Manchester City.
0 comments:
Post a Comment