Image
Image

News Alert: Kaya 100 zimelazimika kukimbia nyumba zao kufuatia kutuama maji ya mvua yaliyochanganyika na kinyesi katika nyumba zao jijini Tanga.


Kaya zaidi ya 100 zimelazimika kukimbia nyumba zao kufuatia kutuama maji ya mvua katika nyumba zao na kusababisha mashimo ya vyoo kuharibiwa vibaya na kumwaga maji taka katika makazi ya watu kwa sababu ya kukosa mifereji ya kusafirisha maji hayo kwenda baharini.
Mwandishi wa Tambarare Halisii ameshuhudia adha hiyo katika maeneo mbali mbali ya kata za Magaoni,Tangasisi na Mabawa ambapo nyumba zaidi ya 100 zimezingirwa na maji yaliyokuwa na vinyesi na kusababisha baadhi ya familia kuhifadhiwa na ndugu , jamaa na majirani kwa hofu ya kutokea kwa magonjwa ya milipuko na kuathiri afya za wakazi wake hasa watoto wa eneo hilo.

Baadhi ya viongozi waliokwenda kufanya ukaguzi katika eneo hilo na kufanya mkutano wa hadhara katika soko la Magaoni, wameiomba serikali kuingilia kati mapema kwa sababu maeneo hayo yamejengwa taasisi za dini zikiwemo madrasa zinazokusanya idadi kubwa ya wanafunzi hali ambayo inaweza kuhatarisha maisha yao.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga, Bwana WINFRED LAZARO amesema halmashauri ya jiji ipo katika mkakati wa kuchimba mfereji wa kudumu kwa ajili ya kupelekea maji hayo baharini hivyo amewaomba wakazi walioathirika na tatizo hilo waendelee kujisitiri kwa ndugu na jamaa hadi suluhisho la kudumu litakapopatikana.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment