Maafisa wa umoja huo wamesema maelfu ya wakimbizi
hao wapo hatarini na ikiwa hatua za haraka hazitachukuliwa huenda idadi ya vofo
ikaongezeka katka siku zijazo.
Wanaothirika zaidi na kipindupindu ni watoto na
wanawake ambao wamekimbia nchi yao kwa hofu ya ukosefu wa usalama.
Mashirika ya Kimataifa kutoka misaada ya kibinadamu
kama OXFAM yamesema wakimbuzi hao wanakosa maji safi ya kunywa pamaja na
ukosefu wa huduma za matibabu.
Hata hivyo wakimbizi kutoka Burundi wanaendelea
kuwasili mjini Kigoma kwa meli wakitokea Kagunda.
Wanapowasili wanapelekwa katika katika kituo cha
muda kabla ya kwenda katika kambi ya Nyaragusu.
Umoja wa Mataifa unasema tayari wakimbizi zaidi ya
elfu hamsini wameingia nchini Tanzania kwa kuhofia usalama wao kutokana na hali
ya kisiasa inayoendelea nchini Burundi.
Hayo yakijiri maandamano yaendelea katika wilaya
mbalimbali za mji wa Bujumbura. Watu waandamanaji wawili waliuawa na polisi
Alhamisi wiki hii. Moja aliuawa katika wilaya ya Musaga kusini mwa jiji la
Bujumbura na mwengine aliuawa wilayani Ngagara kaskazini mwa jiji hilo.
Wakati huo huo Ubelgiji umetangaza kusitisha msaada
wake wa moja kwa moja kwa Burundi.
Kauli hiyo imetolewa na naibu waziri mkuu na waziri
wa ushirikiano wa kimataifa Alexander de Croo akihojiwa na kituo chetu cha
runinga cha France 24.
Ubelgiji ni mfadhili wa kwanza wa Burundi kwa kuipa
kila mwaka msaada wa zaidi ya Euro milioni 47 ambazo zitafadhiliwa kwa njia ya
mashirika yasiyo ya kiserikali na mashirika ya kiraia.
Wakati hayo yakijiri, Mkurugenzi wa kituo cha
binafsi cha Redio na televisheni cha Renaissance Fm anatarajiwa kuwasili leo
Ijumaa kwenye mahakama ya mjini Bujumbura kwa uchunguzi kufuatia harakati za
jaribio la mapinduzi, huku mkurugenzi wa Taasisi ya mawasiliano nchini humo
Richard Giramaho akivitaka vyombo vya habarari kuanza kazi zao kuelekea uchaguzi.
0 comments:
Post a Comment