Image
Image

MADIWANI:Serikali ilipeni halimashauri ya Busega fedha za ushuru wa zao la pamba.


Madiwani katika halimashauri ya wilaya ya Busega mkoani Simiyui wameiomba serikali kuilipa halimashauri hiyo fedha za ushuru wa zao la pamba zilizochukuliwa na Bodi ya Pamba Tanzania ili ziweze kuisaidia halimashauri hiyo katika kumalizia miradi ya maendeleo.

Wakizungumza katika kikao cha baraza hilo ya kujadili hoja za ukaguzi, madiwani hao wamesema pesa hizo kama zitalipwa zitaisadia halimashauri hiyo kukamilisha miradi yake kwani ushuru wa pamba ni moja wapo ya chanzo kikubwa cha mapato ya ndani ya halimashauri hiyo.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkuu wa mkoa wa Simiyu Bwana ELASTON MBWILO amewatoa wasiwasi madiwani hao kwa sababu serikali imeamua kuwa ushuru wa pamba uitalipwa katika halimashauri husika na makampuni yanayonunua pamba, hivyo amewataka madiwani hao kuvuta subira wakati serikali ikishughulikia suala hilo.

Mwaka 2014 iliamua ushuru wa pamba ukusanywe na bodi ya pamba badla ya kulipwas katika halimashauri jambo ambalo lilileta mtafaruku katika halimashauri nyingi hapa nchini husuani zinazolima zao la pamba.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment