Image
Image

SAGINI aweka wazi sababu zinazo sababisha wanafunzi kutoelewa masomo yao na kufeli.


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa -TAMISEMIM Bwana JUMANNE SAGINI amesema kumekuwa na matatizo katika usimamizi wa ufundishaji na ujifunzaji,hali inayosababisha wanafunzi kushindwa kuelewa vyema masomo yao na pia kushindwa kupata stadi na maarifa ipasavyo.
Bwana SAGINI amesema hayo jijini Mwanza wakati akifungua mafunzo kwa walimu wakuu 10,813 pamoja na maofisa elimu wa kata zaidi ya elfu mbili za mikoa 17  ya Tanzania Bara, kuhusu kuimarisha uongozi na menejimenti za shule kupitia kiongozi cha mwalimu mkuu pamoja na miongozo ya kukuza stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu.
Amesema mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka, kufuatia kujitokeza kwa changamoto nyingi za uendeshaji wa shule, ikiwemo uwezo mdogo wa walimu wakuu na mafisa elimu kata kuandaa takwimu za kielimu pamoja na kuwepo kwa walimu waliokata tamaa kutokana na walimu wakuu na maafisa elimu kata kutotimiza wajibu wao wa kusimamia maslahi yao ipasavyo.
Mafunzo hayo yameandaliwa na Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Ofisi ya Waziri Mkuu  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.>>Bonyeza SHARE Hapo juu uwezavyo ili washkaji zako wasipitwe na Stori kama Hizi na Tunapokea matangazo maelekezo hapo kwenye ukurasa wetu yana jieleza kuwa wa kwanza kutangaza nasi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment