Image
Image

Arsenal, Bayern kundi moja UEFA.

Baada ya jana kufanyika droo ya makundi ya klabu bingwa barani Ulaya, mashabiki wa soka watapata fursa ya kushuhudia baadhi ya historia zikijirudia huku zingine mpya zikiandikwa.
Arsenal kwa mara ya tatu katika misimu minne, itavaana na Bayern Munich baada ya kupangwa kundi moja.
Wakati hayo yakijiri, mchezaji mpya wa Manchester Utd Memphis Depay atapata fursa ya kupambana na timu yake ya awali ya PSV Eindhoven ya uholanzi baada ya timu hizo kupangwa kundi moja.
Na ligi kuu ya Hispania La liga, pia mwaka huu imeweka historia baada ya mwaka huu kuingiza timu tano katika hatua hiyo ya makundi, jambo ambalo halikuwahi kutokea hapo awali.
Timu hizo ni Real Madrid, Barcelona, Atletico Madrid, Valencia pamoja na Sevilla.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment