Image
Image

MOI yaelemewa na majeruhi wa ajali za bodaboda.

Idadi ya majeruhi wa ajali za pikipiki wanaopokelewa katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), imekuwa ikiongezeka kwa kasi hadi kufikia 20 mpaka  26 kwa siku sawa na asilimia 53 ya majeruhi wote wa ajali wanaopokelewa katika taasisi hiyo, wakati asilimia 47 wanatokana na ajali nyingine.
Takwimu hizo zinatajwa kuwa ni kubwa ikilinganishwa na majeruhi wa ajali nyingine ambao hupokelewa kwa siku katika taasisi hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada ya Kamati ya Usalama Barabarani Kanda ya Dar es Salaam kufanya ziara na kutoa msaada katika taasisi hiyo, Ofisa Uhusiano wa MOI, Patrick Mvungi, alisema majeruhi wengi wa  ajali wanaofikishwa hapo madereva wa pikipiki na abiria wao na watembea kwa miguu, hali inayosababisha wodi za  wagonjwa hao huzidiwa.
“Katika wodi ya Mwaisela na Sewahaji wanakolazwa majeruhi imezidiwa, kwa mfano, katika wodi ya Mwaisela kuna wagonjwa 54 wakati vitanda ni 33 pekee,” alisema Mvungi. 
Hata hivyo,, Mvungi alisema ujenzi wa jengo jipya kwa ajili ya majeruhi hao upo katika hatua za mwisho na litakapokamilika litakuwa na uwezo wa kulaza wagonjwa 300.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Fadhili Mgonja, alisema ziara hiyo ni muendelezo wa shughuli zinazofanyika katika Wiki ya Usalama Barabarani nchini, ambayo inakwenda sambamba na maonyesho, ukaguzi wa magari na kutoa elimu kwa wananchi juu ya usalama barabarani.
Alisema kutokana na juhudi na ushirikiano wa wadau mbalimbali, ajali hizo zimepungua kwa zaidi ya asilimia 40 ikilinganishwa na mwaka 2013 ambako kulikuwa na vifo zaidi ya 900 vilivyotokana na ajali za barabarani.
Naye Naibu Katibu wa mabalozi wa usalama barabarani, Marlin Komba, alisema wamekuwa wakiendelea kutoa elimu kwa jamii kutii sheria bila shuruti ili kupunguza ajali hizo nchini.
Kumekuwapo na kasi kubwa ya ajali za bodaboda nchini na kusababisha hospitali za serikali kuzidiwa na idadi ya majeruhi.
Hali hiyo imelilazimisha Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha Usalama barabarani kuanzisha kampeni ya kutoa elimu kwa madereva wa bodaboda kwa kushirikiana na taasisi kadhaa kwa lengo la kupunguza ajali hizo.Bofyakujuazaidihttp://bit.ly/1Km9TQU

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment