Sumaye: Kwa ajili ya muda nitasema kwa kifupi
sana, nimetoka chama cha mapinduzi, katibu mkuu alisema sisi ambao
hatukuteuliwa hatukuwa na maadili, mimi nasema kama kipimo cha maadili
ni mheshimiwa Kinana, mimi nitakuwa mtakatifu, CCM wamekuwa wakiongoza
siasa ya chama kimoja kwa ngozi ya vyama vingi, mmekunjika kwa miaka
yote. Tulitaka kufanya mabadiliko kulekule, kukawa na tatizo ndani ya
CCM, ukitaka kufanya lolote wanakuzingira. Wanawajaza watanzania uoga wa
usilolijua, mkiwapa wapinzani wataharibu nchi, kila binadamu ana uoga
wa asilolijua.
Lowassa kwa kuliona hilo, kwa kuwa watanzania wanamfahamu aliona uoga wa
aina hiyo haitakuwepo, na mimi nimekuja kwa sababu hiyo. Watanzania leo
elimu yetu inashuka sana, tunashusha alama za kufaulu wanafunzi
ionekane wamefaulu wengi, pia ukienda katika afya. Tunataka tubadilishe
hali hiyo.
Leo Lowassa ametoka CCM ameonekana hafai, lakini ni KIkwete aliemfanya
waziri mkuu wake, kuna Rais anaweka kiongozi ambae hafai? Lakini ni
LOwassa huyuhuyu ndie aliemuingiza KIkwete Ikulu, Kwamba watanzania
wanampenda Lowassa, halina mjadala.
Mmewasikia kwenye kampeni zao, fisadi mkubwa huyo amechukua fedha za
matajiri, Lowassa amechukua ustaarabu wa kuwajibika. Waziri anachukua
mzigo ili kumuokoa Rais na serikali yake. Asanteni sana.
Nyerere wakati anastaafu, kwenye kikao kimoja nafikiri cha halmashauri
kuu. Alisema hajaona mtu mvumilivu kama Kawawa, alibeba mizigo
aliyostahili kubeba yeye, ndiyo kazi aliyofanya Lowassa. Vichwa vya
treni vinavyonunuliwa, Lowassa alikuwepo? Wajenzi wa barabara nchi hii
wanaidai serikali trilioni 1.4, kudai si tatizo katika hizo bilioni 900
ni pesa za adhabu, huo si ufisadi, mbona hawasemi? Serikali hii ni
dhaifu sana na alituthibitishia katibu mkuu, mwenyewe kusema kuna
mawaziri mizigo.
Mwisho wanalomsema nalo, Escrow Lowassa alikuwepo, kile kipande cha
Lugemalira tulijua waliokula, kila kipande cha Habinder ni nani
aliekula, tangu lini benki ikaruhusiwa kutoa cash kwa mabilioni.
Wamejenga kibr, hawajali tena maumivu ya wananchi, naomba mwaka huu
msikubali, watanzania mfurahie mabadiliko ya ndani ya vyama vingi.
Wanasema mgonjwa, mimi nataka niwaulize, kwani Magufuli mzima? Wanaenda
kufanya nini Ulaya kama ni wazima, mtu yeyote ukishavuka miaka 50
hauwezi kuwa wazima kwa asilimia 100, hivi Rais mkapa alipokuwa
madarakani hakwenda kufanyiwa operashi Ulaya, nchi ilidorora? Alienda
akarudi akaikuta nchi usalama.
Kwani KIkwete alivyokuwa madarakani hakwenda kufanyiwa upasuaji mkubwa
Markani, Rais si kazi ya kubeba zege Ikulu, anatakiwa kuwake timu nzuri
ya kazi, yeye ni meneja tu, naomba sana tumchague itakapofika tarehe 25
Oktoba. Asanteni sana, nawashukuru. Nimkaribishe ndugu Maalim Seif.
Tambwe Hizza: Peoples, kwanza naomba mnisamehe,
mwenzanu nilienda kuongeza ulofa kwenye kiwanda cha ulofa. Watu wazito
wameamua kukiacha chama cha mapinduzi, na mimi nimeamua na wapo wengi
wameogopa eti watasema ana tamaa, hivi nani hana tamaa, hata Magufuli
aliacha ualimu.
Napenda sana Lowassa na Sumaye, juzi nilimuona Rais akifanya utani na
bosi wake, Kikwete akiwa waziri, Sumaye alikuwa waziri mkuu, eti anasema
hajamuelewa, hivi ukishindwa kumuelewa bosi wako utaweza kuwaelewa
watanzania.
Mwakyembe wakati akiwa mwenyekiti wa NBC, Mkapa alipotaka kuuza benki,
Mwakyembe kwa mdomo wake alisema sikubali, leo anatumiwa kuja kumchafua
mheshimiwa Lowassa.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment