Maandalizi ya
uzinduzi wa kampeni za uchaguzi za vyama
vinavyounda UKAWA yanayotarajiwa
kufanyika katika viwanja
vya jangwani yamekamilika.
Kukamilika kwa maandalizi haya
tayari baadhi na makundi
ya wananchi na viongozi kutoka
ndani na nje ya nchi yameshawasili
jijini Dar es Salam kwaajili ya
kuhudhuria hafla hiyo.
Mkuu wa idara ya
mambo ya nje wa UKAWA Bw.Deogratius Mushi amesema asilimia 100 ya maandalizi hayo
yamekamilika tukio hilo litarushwa na vituo
mbalimbali vya Radio na TV za hapa
Tanzania kuanzia majira ya saa nane mchana.
Mushi amesema uzinduzi huo utakuwa ni wa
kihistoria kwani unaonyesha ni jinsi gani watanzania wapo tayari kupokea
mabadiliko na kutoka kwenye mfumo wa chama tawala CCM kilicho kuwa kikishika
dola miaka 50 hadi hivi leo bila ukombozi kwa watanzania ambapo mwanzo huo wa
kesho katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi kupitia UKAWA ndio muendelezo hadi
kushika dola ifikapo Oktoba Asubuhi.Msikie Bw.Deogratius Mushi akieleza namna itakavyokuwa kesho na maandalizi ya jukwaa-Like Page yetu kupata habari.
0 comments:
Post a Comment