Hatua hiyo ya uteketezwaji wa
bidhaa imekuja baada ya TFDA kanda ya kati kufanya ukaguzi katika maduka ya
vinyaji baridi,vipodozi na madawa katika kata tano za manispaa ya Morogoro na
kubaini na kuzikamata bidhaa mbalimbali zilizokuwa zikiuzwa wakati zimewisha
muda wake wa matumizi,ambapo mkaguzi wa TFDA kanda ya kati, Abel deule,amesema bidhaa hizo zilikuwa
zikiuzwa na kutumika kinyume na sheria na kusababisha madhara makubwa ya kiafya
ikiwemo saratani kwa watumiaji,athari kubwa zikiwa ni kwa wanawake na watoto.
Nao wananchi wamesema hatua
iliyochukuliwa na TFDA ni nzuri na fundisho kwa wafanya biashara wanaokiuka
sheria kwa kuuza bidhaa zilizopitwa na wakati,kwa kuangalia zaidi maslahi
yao kuliko kujali afya za watumiaji ambao ni wateja wao.
Kuteketezwa kwa bidhaa hizo
kumekuja wiki mbili tu tangu TFDA kanda ya kati,kuyafungia machinjio ya nyama
katika manispaa ya Morogoro kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kukithiri kwa
uchafu na uchakavu na kutotumika kwa baadhi ya miundo mbinu.
0 comments:
Post a Comment