Image
Image

Jeshi la magereza nchini limefanikiwa kupunguza kero ya mlundikano wa wafungwa na mahabusu katika magereza.


Jeshi la magereza nchini limefanikiwa kupunguza kero ya mlundikano wa wafungwa na mahabusu katika magereza na mahabusu za watoto na hivyo kuipunguzia serikali mzigo wa gharama za kuwahudumia mahabusu na wafungwa  

Akizungumza mjini Morogoro na wasaidizi wa msaada wa kisheria magerezani  kamishina wa sheria na uendeshaji wa magereza dokta juma malewa amesema  kwa muda mrefu  mlundikano wa wafungwa na mahabusu katika magereza ulikuwa kero kwa watuhumiwa  lakini ameshukuru  shirika la enviromental, humani rights care and gender  linalosaidia kutoa elimu ya kishria magerezani kwa kuwaelimisha wafungwa na hatimaye kuwa na uwezo wa kujitetea kwenye mashauri mbalimbali yanayowakabili.
Mkurugenzi wa inviro care bibi  loyce  lema amesema ripoti za wasaidizi wa kisheria magerezani  zimebaini katika magereza  zote nchini wamefungwa kutokana na hali ngumu  ya kiuchumi ambapo wameishauri serika pamoja na taasisi za kiraia  kuelekeza  nguvu katika kuelimisha jamii masuala ya ujasiliamali utakaowawezesha  vijana kujiajiri na kuongeza kipato chao hali hiyo itapunguza  makosa ya uhalifu ili kupunguza mlundikano wa wafungwa magerezani.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment