Image
Image

Wanafunzi wa darasa la saba wasema wanaimani ya kushinda katika mitihani yao.


Wanafunzi wa darasa la saba ambao wanaendelea na mitihani yao ya taifa katika manispaa ya Bukoba, wamesema kuwa wana imani watashinda mtihani huo na kuchaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari.

Wakizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti wanafunzi hao  akiwamo Dorice Prudence wa shule ya msingi Bilele na Lameck Mkayu wa shule ya msingi Rumuli zote za manispaa hiyo, wamesema kuwa wamejiandaa vizuri na wanatarajia kushinda maana walitumia muda wao mwingi kujisomea.

Wamesema kuwa katika masomo ambayo wameanza nayo yamewapa matumaini ya kushinda ,maana waliyofundishwa na walimu wao wameyakuta katika mitihani yao ya kuhitimu darasa la saba.

Wanafunzi hao wametumia fursa hiyo kuwataka watoto wengine wanaoendelea na mitihani hiyo kutulia na kufanya kwa umakini ili waweze kuchaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari kwa manufaa ya maisha yao nay a familia zao ya baadae.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Rumuli Damian Mwesiga amesema kuwa walianza mitihani saa 2 asubuhi na hadi sasa hakuna tatizo lolote liliojitoleza katika shule hiyo.

Mwesiga amesema kuwa kutokana na maandalizi waliyoyafanya kwa wanafunzi wa shule hiyo, ana imani watafanya vizuri na kuendelea kutetea nafasi yao ya ushindi maana katika mtihani kama huo mwaka jana, shule hiyo ilishika nafasi ya kwanza kiwilaya.

Amesema katika shule ya msingi Rumuli ina wanafunzi 121 wanaomaliza darasa la saba mwaka huu wakiwamo wa kiume 56 na wa kike 65.

Naye mwalimu mkuu wa shule ya msingi Bilele Petrades Iganiza amesema kuwa watoto wanaendelea vizuri na mitihani yao maana wanajiamini, wametulia kutokana na kuandaliwa vizuri, na wanatarajia matokeo mazuri.

Iganiza ametumia fursa hiyo kuwataka wazazi wa watoto ambao wanaendelea na masomo shuleni hapo na katika shule nyingine kujitahidi katika kujisomea kwa bidii, ili waweze kufanya vizuri zaidi katika mitihani yao.

Amewataka wazazi kuwanunulia watoto wao vifaa vya shule ikiwamao vitabu, badala ya kutegemea vitabu vya serikali tu ambavyo wakati mwingine havitoshi, ili waweze kufanya vizuri zaidi katika mitihani yao.

Iganiza amesema katika shule yake ya msingi Bilele kuna wanafunzi 47 waliofanya mtihani wao wa taifa wa kuhitimu darasa la saba, ikiwamo wa kiume 18  na wa kike 29.

Afisa elimu wa mkoa wa Kagera, Aloyce Kamamba, amesema kuwa wanafunzi wanaotarajiwa kufanya mtihani huo ni 35,332 wakiwamo wa kiume 16,482 na wa kike 18,850 kutoka katika shule 918 zikiwamo za serikali na binafsi katika mkoa mzima.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment