Image
Image

Wajumbe zaidi ya 80 wa EU kuelekea Burkina Faso kwa ajili ya kufuatilia uchaguzi.


Umoja wa Ulaya (EU) umetangaza mpango wake wa kutuma wajumbe zaidi 80 nchini Burkina Faso kwa ajili ya kusimamia na kufuatilia uchaguzi.
EU ilitoa maelezo siku ya Alhamisi na kusema kwamba wajumbe 24 wataelekea Burkina Faso wiki tatu kabla ya uchaguzi huku wengine zaidi ya 48 wakitarajiwa kuwasili nchini humo siku yauchaguzi.
Msimamizi mkuu wa wajumbe hao wa EU Cecile Kashetu Kyenge tayari amewasili mjini Ouagadougou ili kuanzisha shughuli za maandilizi ya uchaguzi.
Wakati huo huo, EU pia imetoa msaada wa vifaa vya uchaguzi kwa tume ya kitaifa ya kujitegemea ya uchaguzi nchini Burkina Faso.
Uchaguzi uliotarajiwa kufanyika tarehe 11 Oktoba nchini Burkina Faso, ulilazimika kuahirishwa hadi tarehe za mbeleni kutokana na jaribio la mapinduzi lililotekelezwa tarehe 16 Septemba.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment