Image
Image

Sheikh Ponda Ampinga Sheikh Alhad kwa kukataka uchaguzi wa Zanzibar urudiwe.

Kiongozi wa Taasisi na Jumuiya za Kiislam nchini Sheikh Ponda Issa Ponda amepinga uamuzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kurudia uchaguzi visiwani humo.
Amedai kitendo cha ZEC kufuta matokeo ya uchaguzi uliofanyika Octoba 25 mwaka 2015, hakikuwa na sababu za msingi kutokana na uchaguzi huo kufanyika kwa mujibu wa sharia na kanuni za katiba ya Zanzibar.
Ikiwa ni siku moja baada ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kuunga mkono Tume ya Uchaguzi Zanzibar kuhusu kurudiwa kwa Uchaguzi Machi 20, Mwaka huu, Sheikh Ponda amesema kurudia kwa uchaguzi huo si njia sahihi ya kumaliza mgogoro huo.
Amesema Uchaguzi uliofanyika Oktoba 25 mwaka 2015 ulikuwa halali kutokana na taarifa za waangalizi wa ndani na nje ya nchi.
Sheikh Ponda ameungana na viongozi wa Chama cha CUF waliopinga kushiriki marudio ya uchaguzi huo, wakidai Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) wa kufuta matokeo ya uchaguzi huo ni batili kutokana na kasoro nyingi za kikatiba na sheria.
Kwa Mujibu wa Ponda amemwomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo kama alivyoahidi bungeni.
Mwenyekiti wa ZEC, Salim Jecha, alifuta matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 25, 2015 kwa madai kuwa kuna Masanduku ya kupigia kura hayakupewa ulinzi wa kutosha huku baadhi ya maajenti wa vyama pamoja na maafisa wa uchaguzi wakidaiwa kufukuzwa katika vituo kadhaa.
Sababu nyingine zilizotolewa zilikuwa ni kuwepo kwa madai ya Vijana kuvamia vituo vya kupigia kura wakiwa na lengo la kuzua ghasia, na Vyama vya kisiasa kuingilia tume hiyo na kura  kuharibiwa hususan zile kutoka Pemba..
Hata hivyo, licha ya mvutano wa hapa na pale, baadhi ya vyama vya siasa vimekubali kushiriki marudio ya uchaguzi huo, huku wananchi wa Zanzibar wakiombwa kuunga mkono uamuzi huo kwa kujitokeza kwa wingi siku hiyo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment