Image
Image

Wanasayansi wabaini Mate na Mkojo Ndivyo vimesababisha Virusi vya Zika.

Virusi hai vya Zika vyapatikana katika mate na mikojo ya wagonjwa,wanasayansi wa Brazil wamesema.
Matokeo hayo hayamaanishi kwamba ugonjwa huo unaweza kusambazwa kupitia maji maji hayo ya mwilini.Sababu kuu ya kuenea kwa virusi hivyo ni kupitia kuumwa na mbu,lakini wanasayansi wanachunguza njia nyengine.
Huku maambukizi ya Zika yakiwa sio makali,ugonjwa huo umehusishwa na maelfu ya watoto waliozaliwa na kasoro.
Virusi vya Zika pia vimepatikana katika majimaji mengine ya mwilini katika mripuko mwengine uliotokea eneo la Polynesia,lakini mamlaka ya Brazil inasema kuwa hii ni mara ya kwanza virusi hai vya Zika kupatikana.
Paula Gadelha,mkuu wa taasisi ya Fiocruz ambayo inashirikiana na wizara ya Afya amesema:''Virusi hivyo vya Zika vimepatikana katika Mate na mikojo''.
Wanasaynsi wa Brazil
''Lakini hiyo hainamishi kwamba kuna uwezekano wa kuenea kwa virusi hivyo kupitia mate na mikojo.Hatari ya kuenezwa kwa virusi hivyo kupitia maji maji ya mwilini uliangaziwa nchini Marekani ambapo kituo cha udhibiti wa magonjwa kinaamini kisa kimoja kilisambazwa kupitia ngono''.
Hatahivyo kumekuwa na kesi mbili pekee za usambazaji wa virusi hivyo kupitia ngono.



Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment