Image
Image

SUMAYE:Kutokuoneshwa Bunge ni ukiukwaji wa Katiba na kunaminya uhuru wa habari na wananchi kupata habari.

Wakati sekeseke la kutooneshwa mijadala inayoendelea Bungeni kupitia Television(Runinga) ya Taifa TBC LIVE bado linaendelea kuchukua Sura mpya kila uchao ambambo aliyekuwa Waziri mkuu mstaafu nchini Tanzania Frederick Sumaye naye amelaani kitendo hicho nakusema ni ukiukwaji wa haki ya msingi ya kikatiba za kutoonesha Bunge nakuwanyima watanzania haki ya msingi ya kufuatilia mijadala inayoendelea Bungeni.
Mh.Sumaye ameyasema hayo Leo ikiwa nikilele cha Uhuru wa vyombo vya habari duniani ambapo pamoja na mambo mengingine ameonekana kuguswa na kitendo cha matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni kutorushwa kwani wakati yalipokuwa yakirushwa yalikuwa yakiwasaidia wananchi kufahamu na kuyaelewa mambo muhimu yanayohusu nchi, kupata taarifa za maeneo mengine zinazowasilishwa na wabunge na kuona namna ambavyo wawakilishi wao wanavyowawakilisha wakiwa Bungeni mjini Dodoma kwa walicho watuma.
Hata hivyo Sumaye amesema "hatua hiyo inavunja katiba na kuminya baadhi ya taarifa zisiwafikie wananchi na kutoa taarifa ambazo tu utawala umeridhia"Alisema Sumaye.
Aidha ameongeza kwa kusema kuwa kiujumla hali ya vyombo vya habari duniani bado inakutia shaka ambapo takribani wana habari 800 wameuawa duniani ikiwa ni kwa kipindi cha tangu mwaka 2012 mpaka leo, huku wengine wakitekwa au kupotea.
Siku ya uhuru wa vyombo vya
habari duniani ilitangazwa na baraza la umoja wa mataifa mwaka 1993, kwa lengo la kutathimini uhuru wa vyombo vya habari ukoje, kuvilinda vyombo vya habari dhidi ya mashambulizi ya wale wasiotaka maovu yao kufichuliwa na kukumbuka waandishi wa habari waliopoteza maisha yao wakiwa katika kazi zao.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment