Image
Image

Frank-Walter atangaza azma ya nchi yake kuwania kiti katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier ametangaza azma ya nchi yake kuwania tena kiti katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kama mwanachama asiye wa kudumu, kuanzia mwaka 2019 hadi 2020.
Steinmeier aliitangaza azma hizo jana mjini Hamburg, katika hotuba juu ya sera ya uhusiano wa kimataifa. Kwa muda mrefu Ujerumani imetetea mabadiliko katika Baraza la Usalama, ikitaka kupata kiti cha kudumu. Kwa mara ya mwisho Ujerumani ilikuwa mwanachama wa Baraza hilo kati ya mwaka 2011 na 2012.
Kabla ya kura ya kuamua wanachama itakayopigwa mwaka 2018, Ujerumani itaendesha kampeni kuvutia uungwaji mkono wa nchi nyingine. Ombi la Ujerumani litahitaji ridhaa ya angalau theluthi mbili ya wanachama wote 193 wa Umoja wa Mataifa kuweza kufanikiwa.
Ujerumani, kwa ushirikiano na India, Brazil na Japan, zinataka mabadiliko makubwa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, ambalo nchi hizo zinasema limepitwa na wakati.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment