Image
Image

Mahakama ya Afrika ya Haki za binadamu yatoa maamuzi haya.

Mahakama ya Afrika ya Haki za binadamu na Watu  imetoa uamuzi  wa mashauri  manne  yaliyowasilishwa na wananchi wa  mataifa ya Tanzania , Rwanda ,  Bukinafaso  na Libya,  likiwemo  la mtoto  wa aliyekuwa kiongozi wa Libya, hayati   MUAMMAR  GADDAFI  na  mwanasiasa wa Rwanda  VICTORE INGABIRE.
Shauri la raia wa Tanzania,  MOHAMED  ABUBAKAR  linahusiana  na  kesi  ya ujambazi wa  kutumia  silaha  ambalo  mahakama  imetupilia mbali malalamiko  yake   baada  ya kujiridhisha  kwamba  hakukuwa na ukiukwaji  wa  haki za binadamu.
Kwa upande  wa raia wa Rwanda  VICTORE INGABIRE,   mahakama  imeeleza ana haki  ya kusikilizwa  na  kwamba hatua  Rwanda  kujiondoa  kwenye kipengele  cha kuwaruhusu  wananchi  na asasi za kiraia  kupeleka   kesi  kwenye  mahakama hiyo  haiwezi  kuzuia  shauri  hilo  kusikilizwa  na mahakamam  hiyo  ya  Afrika .
Kuhusu   raia wa Bukinafaso  ambeye  ni  Mwandishi  wa Habari,    ISSA  KONETE,  mahakama  imeitaka  serikali  ya nchi hiyo  kumlipa fidi, a baada  ya  kubaini  kuwa  haki zake  zilikiukwa  wakati  kusikiliza  shauri  lake.
Kuhusu  mtoto  wa  aliyekuwa  rais wa  Libya,SEIF GADAFFI ambaye  analalamikia  kukiukwa  kwa  haki  zake,  mahakama  imeitaka Serikali ya Libya kuzifanyia marekebisho baadhi ya  sheria  zinazokiuka  haki  za  binadamu  na  watu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment