Image
Image

UN yasema upo umuhimu mkubwa kutumwa jeshi la ukanda wa Afrika Masariki,Sudani Kusini.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linasema kuna umuhimu mkubwa sana wa kutumwa kwa jeshi la ukanda wa Afrika Mashariki nchini Sudan Kusini.
Rais wa Baraza hilo kwa mwezi wa Januari Olof Skoog, amesema jeshi hilo linahitajika nchini humo haraka iwezekanavyo ili kusaidiana na lile la Umoja wa Mataifa 
kutuliza mapigano yanayoendelea lakini pia kutatua hali mbaya ya kibinadamu nchini humo.
Baraza hilo limesema linasikitishwa sana na mapigano yanayoendelea kushuhudiwa katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo huku maelfu ya raia wa nchi hiyo wakikosa mahitaji muhimu kama chakula, dawa na makaazi baada ya kukimbia vita.
Miezi sita iliyopita, Baraza hilo la UN lilikubali kutumwa kwa kikosi hicho cha wanajeshi 4,000 jiji Juba lakini serikali ya rais Salva Kiir imekuwa ikikataa kuliruhusu kuja kwa jeshi hilo kwa madai kuwa nchi hiyo sasa ina amani.
Rwanda na Ethiopia zinasema ziko tayari kutuma wanajeshi wao katika kikosi hicho cha Umoja wa Mataifa.
Kenya ambayo iliwaondoa wanajeshi wake mwaka uliopita nchini humo, imeiambia Umoja wa Mataifa kuwa inaweza kushiriki katika Operesheni hiyo ikiwa kutakuwa na mazungumzo kati yake na wakuu wa Umoja huo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment