Image
Image

Nape azindua Program ya mfuko wa kusaidia timu za taifa jijini Dar es Salaam.

Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, utamaduni, Sanaa na Michezo Mh.Nape Nnauye amezindua Program ya mfuko wa kusaidia timu za Taifa wenye jukumu la kubuni vyanzo mbalimbali vya rasilimali na kuwataka watanzania kwa umoja wao, Sekta binafsi na familia ya wanamichezo kuunga mkono juhudi hizo.
Akizungumza na wanahabari 23 February 2017 jijini Dar es Salaam Waziri Nape amesema kuwa wao kama serikali na kama sehemu ya wadau hawatasita kusimama hadharani na kunyoosha kidole kama mambo hayataenda sawa, kutokana na wanataka wajenge mfumo ambao wadau watafikia mahali wawaamini kwamba mambo hayo yanasimamiwa na yanaenda vizuri.
Amesema imani ya serikali katika ubunifu huo ni matumaini yao kwamba jambo hilo litakwenda vizuri na kupatikana matokeo wanao yakusudia.
 "Msisite kuchukua hatua mapema pale ambapo kutaonekana hata mashaka kido juu ya utendaji ni vizuri tukachukua hatua mapema ili tusije tukaonekana na sisi ni sehemu ya tatizo, jambo hili zuri likisimamiwa vizuri litatupa matokeo mazuri, jambo hili zuri likisimamiwa vibaya linawezekana likawa ni kaburi la kuzika juhudi mbalimbali zitakazo jitokeza za kujaribu kutafuta fedha yakufainest michezo katika nchi yetu"Nape.
Waziri Nape AmempongezaMkuu wa kitengo cha Maendeleo ya Soka cha Shirikisho la soka Tanzania (TFF).Serengeti Boys Kim Poulsen kwa kazi nzuri anayo fanya pamoja na wenzake, huku akisema kuwa Serengeti Boys wao kama serikali wana matumaini makubwa na timu hiyo kwa kuwa timu ni nzuri na hakuna sababu ya kushindwa.
"Watanzania kwa pamoja tukishikamana tunayotimu nzuri hatunasababu ya kushindwa, watanzania tupunguze tabia ya kunyoosha vidole vibaya, kama kuna mabaya bakinayo moyoni mwako tuseme mema juu ya Serengeti Boys na naamini tutafanikiwa"Nape.
Pia amesema suala hilo serikali haitasita kuingiza mkono kuhakikisha kwa namna yeyote iwe kwa hamasa kwa rasilimali kuwa Serengeti Boys inaenda kupiga kambi na ifanye vizuri kwenye maandalizi yake kwenda Gabon na wanaimani itafanya vizuri.
Ameongeza kwa kusema kuwa alikuwa anaongea na rais wa TFF hivi karibu kwamba serikali itaangalia uwezekano wa kuwa na kamati ya hamasa kwa ajili ya kuhakikisha inasapoti Serengeti Boys na kuhakikisha inafanya vizuri Gabon.
Safari hii haendi mwalimu Posen na watu wake, haiendi Serengeti Boys peke yake, watanzania tunakwenda Gabon,watanzania kwa pamoja, kwa dua zetu kwa rasilimali zetu na kila kitu tunachoweza na hata kamati za ufundi zikiweza lakini kikubwa kuliko yote safari hii watanzani tunataka kwenda gaboni wenyewe tuhakikishe tunarudi na ushindi"Nape.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment