Image
Image

Watoto 600 wapotezana na wazazi wao.


Kigoma.
Zaidi ya watoto 600 wakimbizi kutoka Burundi wamepotezana na wazazi wao katika harakati za kukimbia nchi yao au kuhamishwa kutoka kambi moja kwenda nyingine mkoani Kigoma.
Baadhi ya watoto hao, walipotezana na wazazi wao wakati wa kupanda meli za Mv Liemba na Mv Malagarasi kutokea Burundi na wengine katika harakati za kwenda Kambi ya Nyarugusu.
Toka Mei Mosi, mwaka huu, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) linawasafirisha wakimbizi hao kutoka kambi moja hadi nyingine kwa kutumia meli za Mv Liemba na Mv Malagarasi. Hata hivyo, kutokana na idadi kubwa ya wakimbizi katika kambi zote pamoja na utaratibu mbovu wa kuwahamisha kutoka kambi moja kwenda nyingine.
Mfanyakazi wa Shirika la Uhamiaji la Kimataifa (IOM), Frederick Moses alisema uhamishaji ulikuwa haufuati utaratibu maalumu kwa kuwa meli moja kutoka Kagunga kwenda mjini Kigoma ilikuwa inabeba wanaume tu au wanawake tu na nyingine watoto pekee hali iliyosababisha familia kupotezana.
Takwimu kutoka Ofisi ya Ustawi wa Jamii iliyopo katika kambi ya Uwanja wa Lake Tanganyika, zinaonyesha kuwa Mei 18, mwaka huu, watoto 53 walipotea, Mei 19 walipotea 124, Mei 20 (160), Mei 21 (81), Mei 22 watoto 145 na Mei 24 walipotea watoto zaidi ya 20.
Hata hivyo, Mollel alisema Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na Shirika la Plan International, Unicef na Kamati ya Uokoaji ya Kimataifa (IRC), wanafanya kazi ya kuwatambua watoto waliopotea au waliotengana na wazazi wao na kuwatafutia wazazi wa muda wa kuwalea.
Msemaji wa Plan International, Emmanuel Kihaule alisema watoto hao huhifadhiwa hadi pale wazazi wao watakapopatikana na wale wagonjwa huwekwa katika uangalizi maalumu wa tiba.
“Wapo pia walioathirika kisaikolojia kutokana na kufanyiwa ukatili wa kijinsia, wako kwenye uangalizi maalumu,” alisema.
Baadhi ya watoto hao walisema waliondoka Burundi peke yao huku wengine wakisema walikuwa wanaishi mitaani mjini Bujumbura na waliposikia mapigano wakaamua kufuata mkumbo wa kukimbia.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment