Image
Image

EXCLUSIVE: BILALI AWAASA WAISLAMU, AWATAKA KUWA NA AMANI NA MSHIKAMANO.


Makamu wa Rais Dk.Mohammed Gharib Bilal  amewataka Waislamu  kutambua umuhimu wa kudumisha amani umoja na mshikamano wa watanzania na kuwaonya baadhi ya watu au kikundi cha watu wanaotaka kutumia dini hiyo kuvunja amani ya nchi.

Dk.Mohammed Gharib Bilal - Makamu wa Rais Tanzania. 
Makamu wa Rais ametoa rai hiyo kwenye hotuba yake iliyosomwa na Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe wakati  alipokuwa akifungua kongamano la utamaduni wa kiislamu  lililohusisha masheikh na wanazuoni kutoka nchi tisa za Afrika na Asia.

Amesema utunzaji wa amani ya nchi ni pamoja kuvumiliana na kuheshimiana baina ya watu wa imani ya dini moja dhidi ya nyingine na kwamba kwa kufanya hivyo watakuwa wameenzi  mafundisho ya Mtume Muhammed SAW.

Jumanne Maghembe - Waziri wa Maji Tanzania.
Aidha amewataka Waislamu kufanya kazi kwa bidii na kujiendeleza kielimu kwa ajili ya kuendeleza  utamaduni wa Kiislamu kwa ajili ya kujenga jamii imara kwa ajili ya maendeleo ya watu wote.

Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi na Katibu Mkuu wa Taasisi ya Masheikh na wanazuoni Tanzania Sheikh Khamis Mataka wamehimiza umoja na mshikamano miongoni mwa waislamu pamoja na umuhimu wa kutii na kufuata sheria za nchi.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment