Image
Image

EXCLUSIVE: VIONGOZI WA DINI WAASWA KUZINGATIA MAFUNDISHO YA DINI ZAO BADALA YA KUWA KICHOCHEO CHA KUTENGANISHA JAMII.


Viongozi wa dini wameaswa kuzingatia mafundisho ya dini zao kwa kuwa dini zimeletwa duniani kwa ajili ya kuwaleta pamoja wanadamu badala ya kuwa kichocheo cha kuwatenganisha na kuvuruga amani.

Rai hiyo imetolewa na waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa,SHAMSI VUAI NAHODHA wakati akifungua kongamano la siku mbili la viongozi wa dini lililoitishwa na kamati ya ulinzi na usalama na viongozi wa dini mkoa wa DSM lililoketi kujadili mustakabali wa hali ya amani katika mkoa wa DSM na nchi nzima ambapo ameongeza kuwa uislam na ukristo sio mzigo bali tutumie fursa hizo kutupa tija katika kujiletea maendeleo.
SHAMSI VUAI NAHODHA-WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA

Akimkaribisha mgeni rasmi katika kongamano hilo mkuu wa mkoa wa DSM ambaye pia ni mwenyekiti kamati ya ulinzi na usalama wa mkoa huo SAID MECK SADIKI amehaidi kutimiza wajibu wa serikali wa kusimamia misingi ya sheria na kanuni kwa watu wanaotii amri na mamlaka kwa hekima na busara ili haki ionekane ikitendeka.
SAID MECK SADIKI -MKUU WA MKOA DSM

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment