Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania
(TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mchezaji wa zamani wa timu
za Pan Africans, Simba na Taifa Stars, Abdallah Msamba kilichotokea juzi usiku
(Juni 12 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa
mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Msamba akiwa mchezaji, na baadaye
kocha wa timu kadhaa alitoa mchango mkubwa kwa timu mbalimbali alizochezea na
kufundisha ikiwemo Villa Squad, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
TFF inatoa pole kwa familia ya
marehemu Msamba, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Chama
cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kinondoni (KIFA) na klabu ya Villa Squad na
kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo
mzito.
Maziko ya mchezaji huyo yamefanyika leo katika makaburi ya Ndugumbi jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa
na mamia ya waombolezaji wakiwemo wachezaji wa zamani na viongozi mpira wa
miguu nchini.
Mungu ailaze roho ya marehemu Msamba mahali pema Amina.


0 comments:
Post a Comment