USIKU wa Alhamisi iliyopita, mkazi
wa mtaa wa Malela, Mbagala, Jijini Dar es Salaam, Anna Mbago (35) aliuawa kwa
kunyongwa na mtu aliyeingia chumbani kwake baada ya kutoboa dari.
Inaelezwa kuwa mtu huyo aliingia
kupitia sebuleni, Anna alisikia kishindo, alipotoka chumbani kwenda kuangalia ndipo akakutana na muuaji ambaye
alimnyonga.
Hata hivyo kabla ya umauti, Anna alipiga kelele zilizosababisha
baadhi ya majirani kuizingira nyumba. Kilio chake hakikuzuia asiuawe kwa vile
hata majirani walishindwa kuingia kwa vile nyumba ilikuwa imefungwa; Muuaji
aliendelea kumnyonga hadi kufa licha ya kuomba asiuawe.
Majirani waliosikia kilio cha kuomba msaada waliizingira nyumba hiyo wakihangaika namna ya kuingia ndani bila mafanikio, kwani milango yote ilikuwa imefungwa.
Baadaye walitoa taarifa polisi kupitia kwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Malela, wakati askari wanafika Anna hakuwa anaendelea kupiga kelele za kuomba msaada, huku wengi wakifikiri labda amejificha au amekufa.
Polisi walipoingia walimkuta Anna kwenye korido, akiwa hajitambui, walipompeleka hospitali ndipo ikathibitika kwamba alikuwa amekufa.
Muuaji alikutwa amejificha chooni ndani ya nyumba hiyo, anasema Mkuu wa Upelelezi katika Wilaya ya Kipolisi ya Mbagala, Thobias Walelo.
Polisi wakiri kweli elimu haina mwishoWahenga walisema ‘Elimu haina mwisho’. Usemi huu umethibitika kwa kamanda wa upelelezi wa Wilaya ya kipolisi Mbagala, mkoani Temeke, Jijini Dar es Salaam, Thobias Walelo wakati akizungumzia mauaji ya Anna Mbago (35).
“Unaposikiliza maelezo ya muuaji, ukizingatia mazingira ya tukio, siyo rahisi kuamini kilichotokea, nakiri tukio hili ni la aina yake kwangu, limenidhihirishia kuwa elimu haina mwisho, napaswa kuendelea kujifunza zaidi kama ambavyo wanadamu tunapaswa kuendelea kujifunza bila kuchoka hadi siku ya mwisho wa uhai wetu,”anaeleza ASP Walelo.
Mtuhumiwa akijieleza.“Naitwa (jina tunalo), ninafanya biashara ya sigara, naishi Mbagala” anasema mtuhumiwa wa mauaji hayo akiwa mikononi mwa polisi. MWANANCHI
Majirani waliosikia kilio cha kuomba msaada waliizingira nyumba hiyo wakihangaika namna ya kuingia ndani bila mafanikio, kwani milango yote ilikuwa imefungwa.
Baadaye walitoa taarifa polisi kupitia kwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Malela, wakati askari wanafika Anna hakuwa anaendelea kupiga kelele za kuomba msaada, huku wengi wakifikiri labda amejificha au amekufa.
Polisi walipoingia walimkuta Anna kwenye korido, akiwa hajitambui, walipompeleka hospitali ndipo ikathibitika kwamba alikuwa amekufa.
Muuaji alikutwa amejificha chooni ndani ya nyumba hiyo, anasema Mkuu wa Upelelezi katika Wilaya ya Kipolisi ya Mbagala, Thobias Walelo.
Polisi wakiri kweli elimu haina mwishoWahenga walisema ‘Elimu haina mwisho’. Usemi huu umethibitika kwa kamanda wa upelelezi wa Wilaya ya kipolisi Mbagala, mkoani Temeke, Jijini Dar es Salaam, Thobias Walelo wakati akizungumzia mauaji ya Anna Mbago (35).
“Unaposikiliza maelezo ya muuaji, ukizingatia mazingira ya tukio, siyo rahisi kuamini kilichotokea, nakiri tukio hili ni la aina yake kwangu, limenidhihirishia kuwa elimu haina mwisho, napaswa kuendelea kujifunza zaidi kama ambavyo wanadamu tunapaswa kuendelea kujifunza bila kuchoka hadi siku ya mwisho wa uhai wetu,”anaeleza ASP Walelo.
Mtuhumiwa akijieleza.“Naitwa (jina tunalo), ninafanya biashara ya sigara, naishi Mbagala” anasema mtuhumiwa wa mauaji hayo akiwa mikononi mwa polisi. MWANANCHI


0 comments:
Post a Comment