Image
Image

Tazama picha na maelezo zikionyesha majeruhi wa ajali ya Majinja iliyogongana na lori la mizigo lililokuwa limebeba kontena katika eneo la Changarawe barabara kuu ya Iringa Mbeya



Mwenyekiti wa kamati ya  usalama  barabarani mkoa  wa Iringa  Salim Asas  (kulia)  akimtazama  mmoja kati ya majeruhi  22  waliolazwa katika  Hospitali ya  wilaya ya  Mufindi mkoani Iringa ambao  walipata ajali  mbaya baada ya  basi la majinja lenye namba za usajili T348 CDE kugongana na lori na  kufunikwa na kontena lake jana eneo la Changalawe nje  kidogo ya  mji  wa Mafinga ,katika ajali  hiyo  watu 42  walifariki  dunia. 


Mkuu  wa  mkoa  wa Iringa Amina Masenza  wa  pili kulia akiwa na  viongozi  mbali mbali  wa  tatu ni kamanda  wa polisi mkoa wa Iringa  Ramadhan Mungi , akifuatiwa na mwenyekiti wakamati ya  usalama barabarani mkoa wa Iringa  Salim Asas na mkuu wa wilaya ya  Mufindi Mboni Mhita  jana  walipofika  eneo la  ajali iliyoua 42 na kujeruhi 22 .
Basi la Majinja likiwa limefunikwa na kontena baada ya ajali iliyohusisha basi hilo na Lori baada ya kugongana yso kwa uso Mafinga mkoani Iringa.
Eneo hili ndilo lililo sababisha ajali licha ya Magari hayo kuwa mwendo kasi lakini Mashimo haya yalielezwa kuchangia ajali hiyo.
 Baadhi ya Majeruhi wa ajali hiyo wakiwa wamelala kitandani katika hospitali ya Mufindi iringa kwaajili ya kupatiwa matibabu kufuatia majeraha wakiyoyapata kufuatia ajali hiyo.
 Hili ni Ambulance ilipokuwa katika eneo latukio ikiwa inabeba miili ya watu waliopoteza maisha.
Badhi ya watu katika eneo hilo la tukio wakiwa wanaangalia hali ilivyokuwa huku wakiwa na mshangao na kubaki na sinto amini kwa ajali iliyotokea na kugharimu maisha ya wapendwa wetu 42 Mafinga Mkoani Iringa.
Watu 42 wamepoteza maisha na wengine 23 kujeruhiwa baada ya lori la mizigo kugongana na basi na kontena lililokuwa limebebwa kuangukia gari hilo la abiria, katika ajali ya aina yake iliyotokea eneo la Mafinga Changalawe mkoani Iringa.
Watu 37 waliokuwa kwenye basi hilo la kampuni ya Majinjah Express lililokuwa likitokea Mbeya kwenda Dar es Salaam, walifariki papo hapo na wengine watano kufariki wakiwa Hospitali ya Mafinga. Dereva wa basi na wa lori hilo la kampuni ya Cipex, pia wamefariki.

Shuhuda mmoja wa ajali hiyo, Nyasio Pascal, aliyekuwa akiendesha basi la Saibaba, alisema aliliona lori hilo likijaribu kukwepa mashimo kwenye barabara hiyo ambayo ni nyembamba, na mara likaanza kuyumba kulia na kushoto baada ya kukanyaga shimo na ndipo lilipolifuata basi na kugongana nalo.

Alisema kontena lililokuwa limebebwa na lori hilo, liliangukia juu ya basi na kulikandamiza, jambo ambalo lilisababisha vifo vya watu wengi na pia kuzuia watu waliokuwa karibu na ajali kuokoa watu waliojeruhiwa hadi tingatinga lilipowasili. Hata hivyo, alisema mtoto mmoja mwenye umri wa mwaka mmoja, alinusurika kwenye ajali hiyo bila ya kudhurika.

Miili ya waliokufa imehifadhiwa kwenye Hospitali ya Mafinga, ambayo ina chumba cha kuhifadhia miili ya watu saba tu, na mingine imepelekwa Hospitali ya Rufaa ya Iringa.

“Hii ni ajali mbaya ambayo haijawahi kutokea mkoani hapa,” alisema mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza aliyefika eneo hilo la ajali.

Wanaume saba na wanawake 35 wamepoteza maisha kwenye ajali hiyo, iliyochukua maisha ya watoto watatu.


Katika eneo hilo ambako ajali hiyo imetokea hali ilikuwa mbaya kutokana na kontena la lori hilo kulalia basi na kukandamiza miili ya abiria, jambo ambalo lilisababisha ugumu katika kuokoa abiria waliokuwemo ndani ya basi.

Polisi wakishirikiana na watoa huduma ya afya kutoka Mufindi walifika kusaidia katika kutoa huduma ili kuokoa wale ambao walikuwa wamejeruhiwa na kuhitaji matibabu ya haraka.

Tingatinga lilifika na kusaidia kulinyanyua kontena na hivyo kurahisisha kazi ya kutoa miili ya wale waliokuwa wamebanwa na miili ya waliokufa pia.

Majeruhi wazungumza

Kevin Humprey, aliyekuwa amekaa viti vya nyuma kwenye basi hilo, alisema alisikia kishindo kimetokea na kuona kontena limelalia sehemu kubwa ya basi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment