Mhe.Ndesamburo
ametangaza uamuzi huo kwenye mkutano wa hadhara wa wananchi wa manispaa ya
moshi katika kata ya mbuyuni na kuwashukuru wananchi kwa kumpa ushrikiano
mkubwa kwa miaka yote 15 ya ubunge wake.
Amesema,amechukua uamuzi
huo kuondoa makundi ndani ya chama, majungu na fitina ambazo zilianza
kujitokeza ili kujenga umoja na mshikamano zaidi na amewataka wananchi hao
kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura.

0 comments:
Post a Comment