Wakizungumza katika ofisi za Chadema kanda ya Magharibi mjini
Tabora, viongozi wa Bavicha na Chaso,wameonesha wasiwasi mkubwa wa kudai kuanza
kwa mizengwe ya kunyimwa haki ya kupiga
kura kutokana na mkanganyiko katika fomu ya maombi ya
utambulisho wa mpiga kura inayotolewa na tume ya taifa ya uchaguzi wanazotakiwa
kujaza na wanavyuo,na utaratibu mzima wa zoezi la uchaguzi litavyoendeshwa wakilinganisha
na lile la uchaguzi mkuu wa mwaka 2010
hasa kwa kufungwa vyuo na wanafunzi kurudi makwao maeneo ambayo
kimsingi hawakujiandikishia katika daftari la kudumu la mpiga kura.
Katibu wa Chadema mkoa wa Tabora Bw.Alinanuswe Edson ameiomba
serikali kulishughulukia mapema suala hilo ambalo amedai huenda
likaleta mzozo ambao pengine ukasababisha athari kubwa hususani kwa vijana.
Aidha katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010
baadhi ya wanafunzi wa vyuo imedaiwa kuwa hawakupata fursa ya kupiga
kura ipasavyo kutokana na kuwepo kwa mkanganyiko uliosababishwa
na kuondoka maeneo ambayo walijiandikishia kupiga kura na
hivyo kuleta usumbufu mkubwa katika kuteleza haki hiyo ya kimsingi.




0 comments:
Post a Comment