Viongozi
muhimu wa upinzani nchini Burundi walisema hayo jana katika mkusanyiko wa
wananchi na kuwataka waondokane na woga na kuendeleza maandamano licha ya
kukabiliwa na ukandamizaji unaofanywa na vyombo vya usalama vya nchi hiyo.
Dieudonné Bashirahishize, mmoja wa wawakilishi wa jumuiya za kiaraia nchini
Burundi ameashiria katika mkusanyiko huo juu ya kuuawa raia 20 hadi sasa na
kuwataka wananchi kutolegeza kamba na kupuuza tahadhari iliyotolewa na Baraza
la Usalama wa Taifa la Burundi.
Jana makumi ya vijana waliandamana katika
viunga vya mji mkuu Bujumbura kupinga hatua ya Rais Nkurunziza ya kutangaza nia
yake ya kugombea katika uchaguzi ujao wakisema inapingana na Katiba na ni
kinyume kabisa na makubaliano ya Arusha. Wakati huo huo, duru za habari
zinasema kuwa, tume ya kusimamia uchaguzi nchini humo, imekubali kuakhirisha
uchaguzi wa bunge uliokuwa umepangwa kufanyika terehe 26 ya mwezi huu kwa muda
wa wiki moja mbele.


0 comments:
Post a Comment