Image
Image

News Alert:Dokta Mwakyembe Agadhabishwa na wanao mchafua kupitia mitandao*Asema ameshawabaini wanne*Aonya wale wanao tumia mgongo wake kumchafua.



Waziri wa ushirikiano wa afrika ya mashariki Mh. Harrison Mwakyembe ameeleza kusikitishwa na kufedheheshwa na tabia ya baadhi ya watu kutokuwa majasiri na kutumia majina ya watu wengine kutoa maoni ama misimamo yao kwenye mitandao ya kijamii ambapo ametoa mfano wa jina lake  kutumika kumchafua Mh. Edward Lowasa kuhusu RICHMOND.
Amesema kuwa wapo watu wanaojaribu kutengeneza mambo kusudi kuchafua jina lake hali ambayo haikubaliki hata kidogo huku akisema kwamba suala la Richmond lilishakwisha muda mrefu kwani kazi yake ilikuwa nikuchunguza na kuleta ripoti hivyo anashangaa watu hao wanaoanza kutunga mambo na kusambaza.
Anasema yeye suala lolote analo lishughulikia huwa anajua namna ya kuklikusanyia taarifa na hakuna ubishi huo na mwisho wasiku likaleta majibu mazuri hivyo mtu ambaye anajisikia kukaa tu chini na kutunga mambo na kusambaza hiyo sawa nay eye anasema limemfedhehesha mno mno kwa kuwa halina ukweli.
Kauli yake hii ameitoa wakati wa mahojiano yake na baadhi ya vituo vya Radio na Runginga(TV) jijini Dar es Salaam uliojikita kufahamu ukweli wa taarifa hizo ambazo zimekuwa zikisambaa ambapo Mh.Mwakyembe amekanusha kuhusika na kuongeza kuwa suala hilo si lake bali ni maamuzi ya Bunge na kwamba suala la Richmond lilifungwa miaka saba iliyopita.
Amesema kuhusiana na taarifa hizo zinazo sambaa katika mitandao ya kijamii na hata wakati mwingine kuchapishwa katika baadhi ya magazeti bila kumuhoji hali ambayo inamfanya wakati mwingine kupokea simu kwa watu mbali mbali na wakimuuliza vipi mbona umetumia maneno makali katika taarifa zako katika vyombo vya habari amesema hata yeye amebaki akishangaa kutokana na kwamba taarifa hizo kwake ni mpya.
Mh.Mwakyembe amechukua hatua tayari kuweza kuwabaini wale wanao sambaza taarifa hizo ambapo amesema kuwa amesharipoti kwa vyombo husika hususani jeshi la polisi na mamlaka ya mawasiliano nchini TCRA ambapo tayari wameshabainika baadhi ya watu waliohusika  ambapo baadhi ya watu hao ni viongozi wa dini na wafanyakazi wanaoheshimika katika baadhi ya wizara na kwamba baada ya uchunguzi kukamilika watawekwa hadharani ili liwe fundisho kwa wengine.
Pia Mh.Mwakyembe amesema atahakikisha mara baada ya uchunguzi kukamilika kuweza kuchapisha picha zao katika vyombo vya habari ili watanzania wawatambue,amesema hadi sasa wameshawapata wa nne katika uchunguzi wa awali hivyo watachunguza hadi kupatikana kinara mkuu wa usambazaji wa taarifa hizi.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment