Image
Image

Jokate kutoa somo kwa wasanii leo.


MREMBO na mwanamitindo maarufu nchini, Jokate Mwegelo, leo atatoa somo kwa wasanii na wadau wa sanaa katika kongamano la Jukwaa la Sanaa litakalofanyika kwenye ukumbi wa Basata jijini Dar es Salaam.
Ofisa Habari wa Basata, Aristides Kwizela, alisema Jokate pamoja na mbunifu mashuhuri wa mitindo ya mavazi nchini, Asia Idarous, watatoa mada katika jukwaa hilo na watazungumzia namna ya kutumia umaarufu na vipaji vyao kukuza kipato.
“Jukwaa hili litawataka wasanii na wadu wa sanaa wachakarike, wapate mwanga na namna ya kutumia umaarufu na vipaji walivyonavyo katika kuibua miradi ya ujasiriamali na kujiongezea kipato,” alisema Kwizela.
Alisema wameamua kuweka mada hiyo lengo ni wadau wa sanaa wajifunze kutoka kwa wanamitindo hao wawili ambao wamekuwa na mafanikio makubwa katika kazi zao zinazoendana na umaarufu wao.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment