Image
Image

Toa damu yako kwa bure ili kunusuru maisha: WHO yatoa wito.


Jana tarehe 14 ikiwa ni siku ya utoaji damu duniani, Shirika la Afya Duniani WHO limemulika umuhimu wa watu wanaojitolea ili kuokoa mamilioni ya maisha duniani, kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa ni "Ahsante kwa kunusuru uhai wangu".
Katika mahojiano na redio ya Umoja wa Mataifa, msemaji wa WHO Tarik Jasarevic amesema mwaka 2012, milioni 108 za utoaji damu zimekusanywa, lakini nusu yake ilitokea kwenye nchi zenye kipato cha juu ambapo huishi asilimia 15 tu ya raia duniani.
Bwana Jasarevic ameongeza kuwa, utoaji damu wa kujitolea umeongezeka katika kipindi cha miongo kadhaa iliyopita, lakini bado nchi 72 duniani hushindwa kukusanya damu kupitia utoaji wa kujitolea na hivyo hukusanya damu kupitia utoaji wa kulipwa au familia za wagonjwa.
Msemaji huyu amesema nchi hizo bado zinashindwa kuhakikishia usalama wa upatikanaji wa damu, huku WHO ikieleza kupitia taarifa yake kuwa asilimia 27 ya vifo vya wanawake wajawazito hutokea kwa sababu ya kupoteza damu kupitia kiasi.
WHO inatoa wito kwa kila binadamu kujitolea kutoa damu mara kwa mara.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment